Monday, October 6, 2014

KUMRADHI SANAAAAAA

Kwenu wadau,
Kwa niaba ya timu yangu, nawaombeni radhi sana kwa ukimya uliodumu kwa muda mrefu. Kuna sababu za Msingi zilizosababisha haya yote. Lakini kubwa ni Mkakati mkubwa unaoandaliwa na Msigwa Blog katika kuhabarisha kwa uhakika, upana na undani. Naomba tuendelee kuvuta subira

Gerson Msigwa
DG Msigwablog

Tuesday, May 6, 2014

Wadau tuongeze juhudi kuinadi Tanzania



Ujumbe
Kwa takribani siku tatu nimekua safarini kikazi Pemba na Unguja na kisha Dar es salaam. 
Nadhani wadau bado tuna kazi ya kufanya kuzinadi fursa zilizopo katika maeneo yetu kimkakati. Kwa mfano fukwe zetu bado zinatumia kwa Uchuuzi wa Samaki, Kampuni ya Azam Marine sasa imetatua moja ya kero kubwa zilizokua zikikabili mawasiliano kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar nina maana kero ya Usafiri lakini bado hakuna joto la ushirikiano wa kimanufaa linaloonekana kwa kiasi cha kutosha kwa kutumia fursa hii mfano Ukuzaji Utalii wa Ndani na nje kati ya maeneo haya mawili, Hotel na mengine.

Nimejifunza kuwa Zanzibar bado inahitaji kutangazwa zaidi ya ilivyo sasa, Utamaduni wake, rasilimali zake hasa mazao ya marashi, Utamaduni wake nakadharika. Nimejifunza kuwa wawekezaji katika sekta ya Hotel Zanzibar wanapaswa kufanya zaidi ya ilivyo sasa ili pawe mahali pakukimbiliwa na hata watu wakipato cha Chini badala ya kuwategemea wageni pekee.

Nimejifunza kuwa sisi waandishi wa habari kwa kutumia rungu letu la Utangazaji na uchapishaji tuna kazi kubwa ya kuamsha, kujenga na kuimarisha Utalii wa ndani. tuwajenge watanzania kuwa Mtalii si lazima awe mgeni kutoka nje ya nchi. tunaweza kufanya hili.

Na kwa kuwa wakati huu Tanzania imefunikwa na joto la kuandika Katiba Mpya huku ajenda ya Muungano wa namna gani ikiwa imefunika kazi nzima ya Kuandika Katiba tuna kazi kubwa ya kuwaelimisha watanzania juu ya safari hii ili imalizike kwa usalama. Safari hii iepuka mambo yatakayovuruga maziwa na asali waliyonayo watanzania wa bara na visiwani hata kama wengi wanaona haijawanufaisha wananchi. tuwawezeshe watanzania kupima hoja zinzotolewa ni kwa namna gani fursa hizi zitaathirika ama kupiga hatua.

Muhimu zaidi tufanye kazi hii tukiwa na mawazo huru na kutanguliza maslai ya Taifa Mbele. Najua hapa kuna chngamoto kubwa lakini Mungu aongoze

Gerson

Baada ya Kimya Kirefu

Kutoka kwangu,
Nikiri kwamba nimekua kimya kwa muda mrefu pasi kuweka kitu kipya kwenye Blog
Ahaa kama mnavyojua kubanwa na mengi ndio sababu. Hata hivyo tupo pamoja na tuendelee kuwa pamoja


Thursday, March 6, 2014

Msaada wadau kutambua majina ya wachezaji hawa wa Majimaji FC enzi hizo za Dr Gama

 

Mdau Mpenda Mvula Kanijaalia picha hii ya timu ya Majimaji ya Songea Enzi hizo za Bambo Gama (Dr Laurence Gama) lakini kanipa mtihani kutafuta majina ya kila mchezaji hapo. Msaada wadau.
 
Huyu ni Mzee Abdalah Ally, Mmoja wa waasisi wa timu ya Majimaji. Yeye na wenzake akina Mbegambega walikua na timu zao za soka zilizokua na nguvu Songea, alipokuja Dr Gama akawashawishi wavunje timu zao na kuunda timu ya Majimaji na wao wakawa viongozi. Kuna
habari kuwa Mzee huyu alikua mpenzi Mkubwa wa Majimaji FC kiasi kwamba miaka ya 80 Majimaji ilipofungwa na Yanga alipatwa na Upofu, Namtafuta mwanae Hamis Abdalah Ally athibitishe habari hizi. Mzee huyu ametangulia mbele za Haki Machi 02, 2014
siku ambayo Majimaji ilicheza dhidi ya Lipuli ya Iringa na Lipuli ilichapwa 2-0.
 
 
 


Wadau wajibu wetu uko wapi kwenye hili?

Jamaa jina kampuni akihaha kupiga simu muhimu wakati Mtandao ukiwa unasumbua.
 
 
Hili Tena;
 
Habri wapiganaji wenzangu;
Awali ya yote kwanza poleni kwa kazi na Hongera kwa kulijenga Taifa kwa gharama kubwa.
 
Leo nimeona tukumbushane jambo moja ambalo kwa maoni yangu naona hatuwatendei haki watanzania. Nasema hivi kwa sababu vyombo vya habari ama niseme waandishi wa habari ndio muhimili wa nne wa dola. Kwa lugha nyingine hapa ndio mahali pengine muhimu na pa kipekee ambapo wananchi wanapaswa wapate matumaini na kupaza sauti zao na kukataa kuonewa pale mihimili yote mitatu inayotambuliwa kuwa rasmi inaposhindwa kutimiza matakwa ya wananchi wake.
 
Kuanzia Mwaka jana watanzania wanapata matatizo makubwa ya usumbufu wa kimawasiliano ya simu. Sio kwamba mawasiliano hakuna la hasha, yapo saaana tena hadi vijijini ambako hakukudhaniwa kama ipo siku watu wake watawasiliana na dunia kwa urahisi.
 
Tatizo lililoibuka ni upatikanaji mgumu, ubora wa chini na wakati mwingine kukosekana kabisa kwa mawasiliano ya simu za Mkononi. wapo wanaosema pengine ni kwa sababu makampuni haya sasa yamejikita kwenye huduma za kifedha ndio maana kwenye upigaji wa simu hakutiliwi maanani ya ubora wake.
 
Hebu tufikiria mtu aliyeyapanga maisha yake kwa kutegemea simu ni moja ya nyenzo za kuwezesha mipango yake mawasilaiano yanapokosekana madhara yake nini? aliye na Mgonjwa akashindwa kuita gari kwa ajili ya kumpelaka mgonjwa wake kwa dharula hospitali inakuwaje? vivyo hivyo kwa wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi ma wengineo?
 
Hii leo ukitaka kupiga simu, huna hakika unayempigia kama utampata, na kama ukimpata huna hakika kama ubora wa mawasiliano utakua mzuri. Kila mahali watu wanapopiga simu wanalazimika kupayuka sauti ili kusikika, mara ukipiga simu unayempigia hapatikani hata kama mpo pamoja hapohapo (kama unajaribu), mara ukipiga simu unakutana na kelele za kuudhi.
 
Hii leo watanzania wanapotezewa muda, unapiga simu ili uongee na mtu fulani kwa haraka badala yake unapigiwa matangazo ya biashara kwanza kwa muda mrefu ndipo unajibiwa hapatikani ama unaunganishwa na muhusika.
 
Hii leo, watanzania wangapi wanaingiza vocha kwenye simu zinapotea, na ukifuatilia kwenye madawati ya wateja ya kampuni za simu hakuna msaada.
 
Hii leo makampuni ya simu yote madawati yake ya huduma kwa wateja ukipiga simu ya bure basi unapaswa utenge nusu saa kwa ajili ya kuuliza huduma Fulani ambayo kimsingi ni haki ya mteja na ya bure, tena makampuni mengine yameamua kuwabagua watanzania kuna huduma ya bure ya kusubiri hata saa nzima na kuna huduma ya kulipia.
 
Hii leo Serikali imetangaza kupungua kwa gharama za upigaji wa simu, nani kapunguza gharama hizo? badala yake watanzania wameanzishiwa utamaduni mpya wa kushiriki bahati nasibu ya kampuni za simu, mara tuma ujumbe ushinde milioni 50, nyumba nakadharika. Uhalali wa bahati nasibu hizi anaufuatilia nani, watanzania wanajua kinachofanyika kinaga ubaga?
 
Hii leo mawasiliano ya simu ya Kampuni Fulani yanaweza kukosekana hata siku nzima na watanzania hawaombwi radhi na hakuna fidia. 
 
Hii leo makampuni ya simu yanakusanya marundo ya faida na zote zinaishia kufanya matumizi ambayo hayana uangalizi kama huo uwajibikaji wa kijamii (Social Responsibility) una manufaa kwa watanzania? Hivi Kampuni ya simu kumleta msanii mkubwawa kimarekani na kumlipa mamilioni ya fedha ndio kipaumbele cha watanzania?
 
Yapo mengi yanayoudhi.
 
Mimi sina tatizo na maudhi ya makampuni haya ya simu kwa sababu najua kuwa makampuni haya yanatafuta faida.
 
Hoja yangu ni kwamba wanaofanywa vichwa vya wendawazimu ni watanzania. Kama ndivyo sie vyombo vya habari tumeshiriki vipi kulinyoosha hili?
 
Inawezekana nina majibu kuwa vyombo vyetu vya habari kwa sababu vinanufaika na matangazo ya biashara kutoka makampuni haya ndio maana haviwezi kuyakosea.
 
Sasa ninachojiuliza kwenye hili vipi wadau, tumeshindwa? tumetekwa na maadui? Bloggers msio na matangazo ya kampuni za simu, magazeti yasiyo na matangazo ya makampuni ya simu, Radio na Televisheni hapo vipi?
 
Watanzania wanaumia jamani, vibaya hivyo twende tuseme, hawa jamaa katika maeneo ambayo wapo makini nayo ni kulalamikiwa, wananchi wanalalamika lakini pa kulalamikia wanakosa kwa sababu sisi hatujawawezesha kulalamika. Vyombo vyetu vya habari ndio hivyo vinaogopa kunyea kambi.
 
Je tukae tu kimyaaaaa
 
Ahaaaaaa Jamani sio vizuri, tunakiuka weledi wetu, mbona  taasisi nyingine zikikosea tunaripoti lets do this please.
 
Kwa heriiiiiii
 
 



Siku nzuri niliyokutana na watu muhimu

 Nilipiga boksi na Kaka Zakaria Ngalimanayo, yeye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Klabu ya Wanalizombe Majimaji ya Songea ambayo ipo mawindoni kusaka kurejea Ligi kuu
 
Hapa nilikutana na Sheikh Jamal (Baba Mayasa) pili kulia, anayefuata ni Abdalah dege mmoja wa WanaCCM waliopata kuongoza Chama kwa heshima kubwa na baadaye akastaafu kistaarabu. Na kwanza Shoto ni Mpiganaji ninayemheshimu sana Juma Nyumayo Mwanataaluma mwenzangu.
 


Sunday, March 2, 2014

hufarijika kuwaona wapiganaji wakongwe



Mwandishi wa Habari Mkongwe hapa Nchini Mzee Mbunda wa kwanza kushoto, anafuatiwa na Andrew Kuchonjoma- Mwenyekiti Ruvuma Press Club, Andrew Chatwanga - Katibu Ruvuma Press Club, Nathan Mtega na Zakaria Nachoa - Mkurugenzi Manipsaa Songea
 
 Mpenda Mvula, Mmoja wa wapiganaji wakongwe katika mambo ya Uandishi wa Habari yeye akijikita katika upiga picha, waandishi wa habari wengi wakongwe hapa nchini wanamtambua huyu jamaa na mpaka leo angalia anatupiga jeki wadogo zake. Hongera sana Brother na Baba yetu katika fani, Big Respect



Samahani Wadau kwa kutoaga, sasa Nimerudi


Sunday, February 2, 2014

Mimi na Chama Cha Nani hii tumetimiza umri wa miaka 37.


 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akishangilia pamoja na wana CCM wa Manispaa ya Songea kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi). Mkutano huu ulifanyika katika uwanja wa Kibulang'oma kata ya Lizaboni, Songea Mjini katika Mkoa wa Ruvuma

 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akipongezana na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dr Emmanuel Nchimbi kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi)

 Wana CCM wakishangilia kwa nguvu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambacho sasa kimetimiza miaka 37 tangu kililetwa duniani mwaka 1977

 Mzee Mustafa Songambele mmoja wa waasisi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na mwanachama namba 15 wa Chama cha TANU akiwahusia wana CCM na wananchi wengine wa Songea

 Tunakushukuru Mzee Songambele kwa kutuanzishia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisikika akisema Mwigulu Nchemba. Anayewatazama nyuma ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho.

Dr Emmanuel Nchimbi, Kiongozi wa "Maneno kidogo, Kazi zaidi" akimwaga maelezo juu ya miradi lukuki ya maendeleo aliyowafanyia wananchi wa jimbo lake katika sekta ya Afya, Barabara, Usafi wa Mazingira, Michezo na Elimu. Jamaa alishangiliwa kuwa Jembe tena Jembe la Mpunga

 Mwigulu Nchemba akiwaaga wananchi wa Songea baada ya kuhunguruma katika Jukwaa la Miaka 37 ya tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, Mkutano uliohunguruma katika viwanja vya Kibulang'oma, Lizaboni Mjini Songea. Jamaa ajenda yake kuu ni Uzalendo na Utaifa kwa kila jambo na ndio maana muda wote ni skafu ya Bendera ya Taifa, I like this, Big respect Brother.


Friday, January 24, 2014

Hii imenikumbusha mbali sanaaaaaa

 Kijijini Ilembula, wilaya ya Wanging'ombe bado akina dogo wanalelewa kama ilivyokua mimi..


 Baada ya kumaliza kazi shambani safari ya nyumbani kuwahi ugali

Baba na mwana wakitoka kwenye majukumu.

Tuesday, January 21, 2014

Hongeraaaaa Mpiganaji Juma Nkamia


Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Juma Selemani Nkamia akipokewa na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Clement Mshana, katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Olegabriel

Hongera saaaaana Juma Nkamia.

Najua kwa pongezi hizi wapo ninaowaudhi lakini naomba wadau tujenge utamaduni wa kukubali mafanikio ya binadamu. 

Nampongeza Juma Seleman Nkamia, mwanahabari wa siku nyingi na mbaye pengine amekua kichocheo cha wana habari wengi wanaofanya vizuri hii leo kutokana na umahiri wake wa utangazaji.

Juma umetutoa kimasomaso, umetupa heshima unatuwakilisha. Sina mengi zaidi na sitaki kuzua mjadala naomba niikamilishe furaha yangu kwa kusema Cheza karata yako vizuri utusafishie njia sote tuliofurahi na wasiofurahi. Ukweli ni kwamba wewe ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Kwani kitu gani eheee, Kaji moja bana. Ahahahahaaaaa!!!!!

Wadau tumetimiza wajibu wetu katika hili?


 Soko la wauzaji vyakula la Namtumbo

 Soko la Namtumbo kwa ndani 

 Vitunguu bwelele

 Nyanya, Tangawizi bwelele

 Maharage na njugu bwelele

 Karanga a.k.a Mtesa

 Viazi

Jambo,

Ni matumaini yangu kuwa wapiganaji wenzangu tunaendelea na jukumu letu la kuwatumikia watanzania.
Tuendelee kufanya hivyo licha ya changamoto tunazokutana nazo.

Ndugu zangu nimepita katika Soko la mazao na bidhaa ndogondogo la Namtumbo Mjini Mkoani Ruvuma na nikiwa hapo kengele ikagonga

Imegonga baada ya kushuhudia vilio vya wauzaji wa Matunda, mbogamboga na vyakula vingine wakilia ugumu wa biashara. wanadai  soko huporomoka sana kipindi hiki cha Mvua kwa kuwa wanunuzi wengi huhamia mashambani wakishughulika na kilimo. Bidhaa nilizoziona sokoni ni pamoja na Nyanya, Vitunguu, viazi, mbogamboga na matunda. Staili inayotumia kuuza bidhaa hizi ni ile ile ya hata kabla Tanzania haijapata uhuru, bidhaa zote zingali zinauzwa zikiwa na thamani ya shambani, hazijaongezwa thamani

Kwa hilo nikakumbuka wajibu wetu waandishi wa habari, kwamba katika safari ya kuongeza thamani bidhaa za wakulima wadau mbalimbali wanapaswa kuhusika, kwanza wadau wa maendeleo matharani taasisi za mitaji, wataalamu wa mashine za kusindikia mazao, wataalamu wa kilimo na usindikaji na wengineo ikiwemo serikali. Sio lengo langu kuwajadili hao

Kengele yangu iligonga kwa swali moja kwamba je sisi waandishi wa habari tumetimiza wajibu wetu wa kuwasaidia wakulima wa Tanzania kuanza na kuchochea safari ya kuongeza thamani ya mazao yao? tumewaonesha fursa zilizopo? tumewaonesha pa kuanzia? Kama tumefanya inatosha? Na kama inatosha tumepima utekelezaji wake na matokeo yake? Na je tunawakumbusha wadau wengine juu ya wajibu huu? kama tumefanya inatosha? Na pia je tumepambana kidete kama tunavyopambana katika masuala ya wanasiasa?

Sio lengo langu kutaka tujilaumu bali kukumbushana kuwa huu ni wajibu mwingine tunaoweza kuwasaidia wakulima. Nafahamu yapo maeneo mengi ya nchi hii yenye shida hii. Naomba tulione hili na tuamue kulivalia njuga. tusipofanya hivi watanzania hasa walala hoi wanaendelea kuumia. Tupige kelele watanzania wale Nyanya za Tanzania popote walipo badala ya baadhi ya watanzania ama watu wanaokuja nchini kwetu kununua nyanya kutoka nje ya nchi. Na sio kwa nyanya tu hata bidha nyingine. Huu ni wakati wa Mvua embe kiasi gani za wakulima zimeoza vijijini kwa kukosa kusindikwa? mbogamboga kiasi gani zinatupwa ama kuachwa ziharibika mashambani?

Tuamue tunaweza kwani sisi ni mhimili wa nne wa Dola japo sio rasmi

Natoa hoja

Sunday, December 29, 2013

Niko sawa, ila kwa sasa nje ya uwanja miezi mitatu

Ball control 100% Super, chezea mimi!??

Hongera Majjid Mjengwa, Wadau sisi vipi?




Hongera Majjid Mjengwa,

Wiki hii inayomalizika mdau mwenzetu katika tasnia ya habari, mchambuzi mkongwe, mwandishi kindakindaki, mfuatiliaji na mdadavuaji wa habari na matukio na mengine mengi Majjid Mjengwa ameweka sokoni kitabu chake kinachomuelezea gwiji wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi na mpigania ukombozi wa Taifa la Afrika ya Kusini, Hayati Mzee Nelson Rolihlahla Mandela.

Mjengwa ameandika kitabu hiki wakati muafaka na amewatendea haki wanajamii hasa wale ambao ama kwa sababu za umri, zama, ama kwa sababu ya kukosa fursa ama kwa sababu nyingine hawakupata kujua kuhusu mwanasiasa huyo Mkongwe alivyojitolea maisha yake kuipigania Afrika ya Kusini iliyokua imetumbukia katika janga la ubaguzi wa rangi ulioendeshwa na makaburu.

Ni sawa Mjengwa ameandika mengi yenye manufaa kwa jamii na ndivyo alivyo kwa tunayefuatilia maisha yake ya uandishi.

Lakini mimi nimeona katika Blog hii Nimpongeze Ndugu Mjengwa kwa sababu alichokifanya ni wajibu wa kila mtu aliyehifadhi historia, taaluma na fursa ya kukiunganisha kizazi cha sasa  na yale yaliyojiri kabla yake.

Katikati ya mwaka 2013 nilihudhuria kongamonano moja lililomwalika Askofu Mstaafu Norbert Mtega katika Jubilei ya kumpongeza Padre Christian Mhagama mmoja wa waandishi wazuri wa vitabu, Askofu Mtega katika Siku hii alisema “Msomi asiyeandika vitabu ni sawa na Mama mjamzito asiyezaa”

Kwa maana hii Mjengwa na waandishi wengine wa vitabu wanatimiza wajibu wao, na wale wasiofanya hivyo wakati wana taaluma ya kufanya hivyo hawatimizi wajibu wao.

Japo kuwa sijapata nakala ya kitabu cha simulizi za Mzee Mandela cha Mjengwa, mimi ni mmoja wa wasomaji wa Blog ya Mjengwa kila uchao na nimefuatilia maandalizi yake kwa kuwa alikua akiweka kwenye Blog yake kila anapofanya tafsiri ya kile kitabu cha Mzee Madiba cha safari ya Ukombozi yaani “Long work to Freedom” Kwa kweli nikiri kuwa hata mimi sijakisoma kitabu hicho cha Madiba na hivyo nilivutiwa mno na simulizi iliyokua ikitafsiriwa na Mjengwa kwenye Blog yake.

Kuna mengi ya kuyasema lakini katika pongezi nimalizie kwa kusema Hongera sana Mjengwa na hongera kwa kuona umuhimu wa kuchapisha kitabu ili iwe kumbukumbu sahihi kwa kila anayetaka kusoma Simulizi za Mzee Mandela na endelea kufanya hivyo kwa mambo mengine mengi yaliyo hazina kwenye kichwa chako kama ilivyo kwaida yako.

Wadau sisi vipi?

Nauliza swali hili kwa sababu naamini kuwa wengi wanaweza kufanya kama alivyofanya Majjid Mjengwa katika simulizi za Mzee Madiba. Hasa kwa sisi waandishi wa habari na katika hili nawagusa zaidi waandishi wa habari wakongwe ambao mimi naamini wana mambo mengi mazuri ya kukisimulia kizazi hiki cha leo hapa Tanzania kuliko watu wengine.

Ndio, wanahabari tunayo fursa hii kwa sababu tunaona mengi. Najiuliza hapa Tanzania Mwalimu Nyerere amefanya mengi katika kupigania uhuru, kuijenga Tanganyika, kuiunganisha Tanganyika na Zanzibar na mengine mengi. Yapo yaliyokua kama vitimbwi, yapo yaliyoonesha uthubutu wa hali ya juu, yapo yaliyoonesha kujitolea hata kufa, yapo yaliyoonesha ujasiri ambao unaonekana leo kama vitu visivyowezekana na mengine kibao.

Haya yote yalifanyika mbele ya waandishi wa habari. Jamani tupeni utamu, tupeni historia, achieni kalamu zenu zitembee, msiache uhondo huo uteketee, msisubiri waje wazungu watafiti ndio waandike.

Akina Mzee Abdul Ngalawa, Ahamed Kipozi, Jenerali Ulimwengu, Phili Karashani, Ernest Mrutu, Agustino Mbunda, Ben Kiko, Hamza Kasongo, Mhidin Michuzi na wengine wengi tupeni uhondo.

Si lazima kutafsiri vitabu lakini zipo simulizi kuhusu yale mliyoyaona wakati huo, jinsi nchi ilivyoendeshwa, jinsi mabadiliko yalivyokuja na mengine mengi.

Sisemi kwamba hamjafanya kabisa hapana, najua baadhi huandaa vipindi, huandika makala na kufanya mahojiano lakini isiishie hapo, tuandikieni vitabu, vitangazeni ili watanzania wavinunue na waijue nchi yao ilikotoka. Jenerali Ulimwengu nakupongeza pia kwa kuwa umetekeleza hili.

Nasema hivi kwa sababu naamini kuwa, baadhi ya matatizo yanayotukumba sasa Tanzania yanaweza kutatuliwa kwa nguvu ndogo tu ya sisi wanahabari kutumia kalamu zetu kuwapata taarifa watanzania, kuwakumbusha watanzania na kuwaonesha njia ya kupita.

Leo hii inashangaza kumuona mtanzania akitoa kipaumbele kwa mambo ambayo yanaibomoa nchi, yanavuruga moyo wa kuijenga nchi kwa kujitolea, yanajenga chuki, yanaruhusu wabaya kuivuruga nchi. Tulikotoka haikua hivyo, na nchi za wenzetu kama vile China bado wanafanya yale ambayo sie tulikua tunayafanya kabla ya miaka ya 90.

Najua aya hiyo hapo juu itakua imewachefua baadhi ya watu, lakini niseme sababu hizo zinazotumiwa na baadhi yetu kuhalalisha mambo yanayoigharimu nchi utatuzi wake unapaswa kutenganishwa na jukumu la msingi la kujenga Taifa letu.

Kama kuna wezi, mafisadi ama walafi tuwaache washughulikiwe na vyombo husika. Wasiohusika tukazane kujenga nchi, haiwezekani sote tukawa walalamikaji, sote tunatafuta wala rushwa na wezi na mwisho wa siku sote tukawa wanasiasa. Nchi atajenga nani?

Jamani eheee wakongwe wa Habari andikeni vitabu watanzania wasome enzi za mwalimu watanzania waliishi vipi?

Na je wala rushwa hawakuwepo?

Mafisadi hawakuwepo?

Viongozi legelege hawakuwepo?

Siasa hazikuwepo?

Waaminisheni watanzania kuwa kila mtu anaweza kuwa mpigania nchi yake na akawa shujaa, kama ambavyo Mjengwa amemuandika Mzee Madiba na simulizi nyingi nyingi alizowahi kuandika.


Mwisho nawapenda sana na niliyoandika sio msahafu. 


Tuesday, December 24, 2013

Kwa muda nyumbani Ilembula

 Brigedi Kamanda wangu, Mwite Chester katika pozi pande za Njombe Town
 Babu, wajukuu na Mkamwana. Kutoka Shoto Chester, Wayne, Mzee Partinus Msigwa na My wife wangu nani hiii ahaaa nani huyuuuu, nani hii ntawambia baadaye.
 Mimi na Ka’Fulo
 Wayne na Bibi Mlangadu
 Mimi na Bibi Mlangadu na Cathy Mgunda
 Bibi Agnes Mlangadu akiwa mwenye furaha
 Mama Semahuvi
Mama yangu Mzazi Paskalina Mahuve a.k.a “Semahuvi” akikamilisha mawasiliano ya mambo Fulani ya kula bata kwa wajukuu zake

MERRY CHRISTMAS



Wadau tusherehekee kwa amani upendo na Mshikamano. 
Nawapenda Nyote Mle, Mnywe na nani hiiiiii pia 

Friday, December 20, 2013

Bungeni Kimenuka TBC Live kutoka Mjengoni

Jamani angalieni wenyewe msisubiri kusimuliwa maana baada ya hapa wapo watakaotia chumvi