Sunday, February 2, 2014

Mimi na Chama Cha Nani hii tumetimiza umri wa miaka 37.


 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akishangilia pamoja na wana CCM wa Manispaa ya Songea kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi). Mkutano huu ulifanyika katika uwanja wa Kibulang'oma kata ya Lizaboni, Songea Mjini katika Mkoa wa Ruvuma

 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akipongezana na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dr Emmanuel Nchimbi kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi)

 Wana CCM wakishangilia kwa nguvu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambacho sasa kimetimiza miaka 37 tangu kililetwa duniani mwaka 1977

 Mzee Mustafa Songambele mmoja wa waasisi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na mwanachama namba 15 wa Chama cha TANU akiwahusia wana CCM na wananchi wengine wa Songea

 Tunakushukuru Mzee Songambele kwa kutuanzishia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisikika akisema Mwigulu Nchemba. Anayewatazama nyuma ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho.

Dr Emmanuel Nchimbi, Kiongozi wa "Maneno kidogo, Kazi zaidi" akimwaga maelezo juu ya miradi lukuki ya maendeleo aliyowafanyia wananchi wa jimbo lake katika sekta ya Afya, Barabara, Usafi wa Mazingira, Michezo na Elimu. Jamaa alishangiliwa kuwa Jembe tena Jembe la Mpunga

 Mwigulu Nchemba akiwaaga wananchi wa Songea baada ya kuhunguruma katika Jukwaa la Miaka 37 ya tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, Mkutano uliohunguruma katika viwanja vya Kibulang'oma, Lizaboni Mjini Songea. Jamaa ajenda yake kuu ni Uzalendo na Utaifa kwa kila jambo na ndio maana muda wote ni skafu ya Bendera ya Taifa, I like this, Big respect Brother.


Friday, January 24, 2014

Hii imenikumbusha mbali sanaaaaaa

 Kijijini Ilembula, wilaya ya Wanging'ombe bado akina dogo wanalelewa kama ilivyokua mimi..


 Baada ya kumaliza kazi shambani safari ya nyumbani kuwahi ugali

Baba na mwana wakitoka kwenye majukumu.

Tuesday, January 21, 2014

Hongeraaaaa Mpiganaji Juma Nkamia


Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Juma Selemani Nkamia akipokewa na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Clement Mshana, katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Olegabriel

Hongera saaaaana Juma Nkamia.

Najua kwa pongezi hizi wapo ninaowaudhi lakini naomba wadau tujenge utamaduni wa kukubali mafanikio ya binadamu. 

Nampongeza Juma Seleman Nkamia, mwanahabari wa siku nyingi na mbaye pengine amekua kichocheo cha wana habari wengi wanaofanya vizuri hii leo kutokana na umahiri wake wa utangazaji.

Juma umetutoa kimasomaso, umetupa heshima unatuwakilisha. Sina mengi zaidi na sitaki kuzua mjadala naomba niikamilishe furaha yangu kwa kusema Cheza karata yako vizuri utusafishie njia sote tuliofurahi na wasiofurahi. Ukweli ni kwamba wewe ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Kwani kitu gani eheee, Kaji moja bana. Ahahahahaaaaa!!!!!

Wadau tumetimiza wajibu wetu katika hili?


 Soko la wauzaji vyakula la Namtumbo

 Soko la Namtumbo kwa ndani 

 Vitunguu bwelele

 Nyanya, Tangawizi bwelele

 Maharage na njugu bwelele

 Karanga a.k.a Mtesa

 Viazi

Jambo,

Ni matumaini yangu kuwa wapiganaji wenzangu tunaendelea na jukumu letu la kuwatumikia watanzania.
Tuendelee kufanya hivyo licha ya changamoto tunazokutana nazo.

Ndugu zangu nimepita katika Soko la mazao na bidhaa ndogondogo la Namtumbo Mjini Mkoani Ruvuma na nikiwa hapo kengele ikagonga

Imegonga baada ya kushuhudia vilio vya wauzaji wa Matunda, mbogamboga na vyakula vingine wakilia ugumu wa biashara. wanadai  soko huporomoka sana kipindi hiki cha Mvua kwa kuwa wanunuzi wengi huhamia mashambani wakishughulika na kilimo. Bidhaa nilizoziona sokoni ni pamoja na Nyanya, Vitunguu, viazi, mbogamboga na matunda. Staili inayotumia kuuza bidhaa hizi ni ile ile ya hata kabla Tanzania haijapata uhuru, bidhaa zote zingali zinauzwa zikiwa na thamani ya shambani, hazijaongezwa thamani

Kwa hilo nikakumbuka wajibu wetu waandishi wa habari, kwamba katika safari ya kuongeza thamani bidhaa za wakulima wadau mbalimbali wanapaswa kuhusika, kwanza wadau wa maendeleo matharani taasisi za mitaji, wataalamu wa mashine za kusindikia mazao, wataalamu wa kilimo na usindikaji na wengineo ikiwemo serikali. Sio lengo langu kuwajadili hao

Kengele yangu iligonga kwa swali moja kwamba je sisi waandishi wa habari tumetimiza wajibu wetu wa kuwasaidia wakulima wa Tanzania kuanza na kuchochea safari ya kuongeza thamani ya mazao yao? tumewaonesha fursa zilizopo? tumewaonesha pa kuanzia? Kama tumefanya inatosha? Na kama inatosha tumepima utekelezaji wake na matokeo yake? Na je tunawakumbusha wadau wengine juu ya wajibu huu? kama tumefanya inatosha? Na pia je tumepambana kidete kama tunavyopambana katika masuala ya wanasiasa?

Sio lengo langu kutaka tujilaumu bali kukumbushana kuwa huu ni wajibu mwingine tunaoweza kuwasaidia wakulima. Nafahamu yapo maeneo mengi ya nchi hii yenye shida hii. Naomba tulione hili na tuamue kulivalia njuga. tusipofanya hivi watanzania hasa walala hoi wanaendelea kuumia. Tupige kelele watanzania wale Nyanya za Tanzania popote walipo badala ya baadhi ya watanzania ama watu wanaokuja nchini kwetu kununua nyanya kutoka nje ya nchi. Na sio kwa nyanya tu hata bidha nyingine. Huu ni wakati wa Mvua embe kiasi gani za wakulima zimeoza vijijini kwa kukosa kusindikwa? mbogamboga kiasi gani zinatupwa ama kuachwa ziharibika mashambani?

Tuamue tunaweza kwani sisi ni mhimili wa nne wa Dola japo sio rasmi

Natoa hoja

Sunday, December 29, 2013

Niko sawa, ila kwa sasa nje ya uwanja miezi mitatu

Ball control 100% Super, chezea mimi!??

Hongera Majjid Mjengwa, Wadau sisi vipi?




Hongera Majjid Mjengwa,

Wiki hii inayomalizika mdau mwenzetu katika tasnia ya habari, mchambuzi mkongwe, mwandishi kindakindaki, mfuatiliaji na mdadavuaji wa habari na matukio na mengine mengi Majjid Mjengwa ameweka sokoni kitabu chake kinachomuelezea gwiji wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi na mpigania ukombozi wa Taifa la Afrika ya Kusini, Hayati Mzee Nelson Rolihlahla Mandela.

Mjengwa ameandika kitabu hiki wakati muafaka na amewatendea haki wanajamii hasa wale ambao ama kwa sababu za umri, zama, ama kwa sababu ya kukosa fursa ama kwa sababu nyingine hawakupata kujua kuhusu mwanasiasa huyo Mkongwe alivyojitolea maisha yake kuipigania Afrika ya Kusini iliyokua imetumbukia katika janga la ubaguzi wa rangi ulioendeshwa na makaburu.

Ni sawa Mjengwa ameandika mengi yenye manufaa kwa jamii na ndivyo alivyo kwa tunayefuatilia maisha yake ya uandishi.

Lakini mimi nimeona katika Blog hii Nimpongeze Ndugu Mjengwa kwa sababu alichokifanya ni wajibu wa kila mtu aliyehifadhi historia, taaluma na fursa ya kukiunganisha kizazi cha sasa  na yale yaliyojiri kabla yake.

Katikati ya mwaka 2013 nilihudhuria kongamonano moja lililomwalika Askofu Mstaafu Norbert Mtega katika Jubilei ya kumpongeza Padre Christian Mhagama mmoja wa waandishi wazuri wa vitabu, Askofu Mtega katika Siku hii alisema “Msomi asiyeandika vitabu ni sawa na Mama mjamzito asiyezaa”

Kwa maana hii Mjengwa na waandishi wengine wa vitabu wanatimiza wajibu wao, na wale wasiofanya hivyo wakati wana taaluma ya kufanya hivyo hawatimizi wajibu wao.

Japo kuwa sijapata nakala ya kitabu cha simulizi za Mzee Mandela cha Mjengwa, mimi ni mmoja wa wasomaji wa Blog ya Mjengwa kila uchao na nimefuatilia maandalizi yake kwa kuwa alikua akiweka kwenye Blog yake kila anapofanya tafsiri ya kile kitabu cha Mzee Madiba cha safari ya Ukombozi yaani “Long work to Freedom” Kwa kweli nikiri kuwa hata mimi sijakisoma kitabu hicho cha Madiba na hivyo nilivutiwa mno na simulizi iliyokua ikitafsiriwa na Mjengwa kwenye Blog yake.

Kuna mengi ya kuyasema lakini katika pongezi nimalizie kwa kusema Hongera sana Mjengwa na hongera kwa kuona umuhimu wa kuchapisha kitabu ili iwe kumbukumbu sahihi kwa kila anayetaka kusoma Simulizi za Mzee Mandela na endelea kufanya hivyo kwa mambo mengine mengi yaliyo hazina kwenye kichwa chako kama ilivyo kwaida yako.

Wadau sisi vipi?

Nauliza swali hili kwa sababu naamini kuwa wengi wanaweza kufanya kama alivyofanya Majjid Mjengwa katika simulizi za Mzee Madiba. Hasa kwa sisi waandishi wa habari na katika hili nawagusa zaidi waandishi wa habari wakongwe ambao mimi naamini wana mambo mengi mazuri ya kukisimulia kizazi hiki cha leo hapa Tanzania kuliko watu wengine.

Ndio, wanahabari tunayo fursa hii kwa sababu tunaona mengi. Najiuliza hapa Tanzania Mwalimu Nyerere amefanya mengi katika kupigania uhuru, kuijenga Tanganyika, kuiunganisha Tanganyika na Zanzibar na mengine mengi. Yapo yaliyokua kama vitimbwi, yapo yaliyoonesha uthubutu wa hali ya juu, yapo yaliyoonesha kujitolea hata kufa, yapo yaliyoonesha ujasiri ambao unaonekana leo kama vitu visivyowezekana na mengine kibao.

Haya yote yalifanyika mbele ya waandishi wa habari. Jamani tupeni utamu, tupeni historia, achieni kalamu zenu zitembee, msiache uhondo huo uteketee, msisubiri waje wazungu watafiti ndio waandike.

Akina Mzee Abdul Ngalawa, Ahamed Kipozi, Jenerali Ulimwengu, Phili Karashani, Ernest Mrutu, Agustino Mbunda, Ben Kiko, Hamza Kasongo, Mhidin Michuzi na wengine wengi tupeni uhondo.

Si lazima kutafsiri vitabu lakini zipo simulizi kuhusu yale mliyoyaona wakati huo, jinsi nchi ilivyoendeshwa, jinsi mabadiliko yalivyokuja na mengine mengi.

Sisemi kwamba hamjafanya kabisa hapana, najua baadhi huandaa vipindi, huandika makala na kufanya mahojiano lakini isiishie hapo, tuandikieni vitabu, vitangazeni ili watanzania wavinunue na waijue nchi yao ilikotoka. Jenerali Ulimwengu nakupongeza pia kwa kuwa umetekeleza hili.

Nasema hivi kwa sababu naamini kuwa, baadhi ya matatizo yanayotukumba sasa Tanzania yanaweza kutatuliwa kwa nguvu ndogo tu ya sisi wanahabari kutumia kalamu zetu kuwapata taarifa watanzania, kuwakumbusha watanzania na kuwaonesha njia ya kupita.

Leo hii inashangaza kumuona mtanzania akitoa kipaumbele kwa mambo ambayo yanaibomoa nchi, yanavuruga moyo wa kuijenga nchi kwa kujitolea, yanajenga chuki, yanaruhusu wabaya kuivuruga nchi. Tulikotoka haikua hivyo, na nchi za wenzetu kama vile China bado wanafanya yale ambayo sie tulikua tunayafanya kabla ya miaka ya 90.

Najua aya hiyo hapo juu itakua imewachefua baadhi ya watu, lakini niseme sababu hizo zinazotumiwa na baadhi yetu kuhalalisha mambo yanayoigharimu nchi utatuzi wake unapaswa kutenganishwa na jukumu la msingi la kujenga Taifa letu.

Kama kuna wezi, mafisadi ama walafi tuwaache washughulikiwe na vyombo husika. Wasiohusika tukazane kujenga nchi, haiwezekani sote tukawa walalamikaji, sote tunatafuta wala rushwa na wezi na mwisho wa siku sote tukawa wanasiasa. Nchi atajenga nani?

Jamani eheee wakongwe wa Habari andikeni vitabu watanzania wasome enzi za mwalimu watanzania waliishi vipi?

Na je wala rushwa hawakuwepo?

Mafisadi hawakuwepo?

Viongozi legelege hawakuwepo?

Siasa hazikuwepo?

Waaminisheni watanzania kuwa kila mtu anaweza kuwa mpigania nchi yake na akawa shujaa, kama ambavyo Mjengwa amemuandika Mzee Madiba na simulizi nyingi nyingi alizowahi kuandika.


Mwisho nawapenda sana na niliyoandika sio msahafu. 


Tuesday, December 24, 2013

Kwa muda nyumbani Ilembula

 Brigedi Kamanda wangu, Mwite Chester katika pozi pande za Njombe Town
 Babu, wajukuu na Mkamwana. Kutoka Shoto Chester, Wayne, Mzee Partinus Msigwa na My wife wangu nani hiii ahaaa nani huyuuuu, nani hii ntawambia baadaye.
 Mimi na Ka’Fulo
 Wayne na Bibi Mlangadu
 Mimi na Bibi Mlangadu na Cathy Mgunda
 Bibi Agnes Mlangadu akiwa mwenye furaha
 Mama Semahuvi
Mama yangu Mzazi Paskalina Mahuve a.k.a “Semahuvi” akikamilisha mawasiliano ya mambo Fulani ya kula bata kwa wajukuu zake