Thursday, March 6, 2014

Wadau wajibu wetu uko wapi kwenye hili?

Jamaa jina kampuni akihaha kupiga simu muhimu wakati Mtandao ukiwa unasumbua.
 
 
Hili Tena;
 
Habri wapiganaji wenzangu;
Awali ya yote kwanza poleni kwa kazi na Hongera kwa kulijenga Taifa kwa gharama kubwa.
 
Leo nimeona tukumbushane jambo moja ambalo kwa maoni yangu naona hatuwatendei haki watanzania. Nasema hivi kwa sababu vyombo vya habari ama niseme waandishi wa habari ndio muhimili wa nne wa dola. Kwa lugha nyingine hapa ndio mahali pengine muhimu na pa kipekee ambapo wananchi wanapaswa wapate matumaini na kupaza sauti zao na kukataa kuonewa pale mihimili yote mitatu inayotambuliwa kuwa rasmi inaposhindwa kutimiza matakwa ya wananchi wake.
 
Kuanzia Mwaka jana watanzania wanapata matatizo makubwa ya usumbufu wa kimawasiliano ya simu. Sio kwamba mawasiliano hakuna la hasha, yapo saaana tena hadi vijijini ambako hakukudhaniwa kama ipo siku watu wake watawasiliana na dunia kwa urahisi.
 
Tatizo lililoibuka ni upatikanaji mgumu, ubora wa chini na wakati mwingine kukosekana kabisa kwa mawasiliano ya simu za Mkononi. wapo wanaosema pengine ni kwa sababu makampuni haya sasa yamejikita kwenye huduma za kifedha ndio maana kwenye upigaji wa simu hakutiliwi maanani ya ubora wake.
 
Hebu tufikiria mtu aliyeyapanga maisha yake kwa kutegemea simu ni moja ya nyenzo za kuwezesha mipango yake mawasilaiano yanapokosekana madhara yake nini? aliye na Mgonjwa akashindwa kuita gari kwa ajili ya kumpelaka mgonjwa wake kwa dharula hospitali inakuwaje? vivyo hivyo kwa wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi ma wengineo?
 
Hii leo ukitaka kupiga simu, huna hakika unayempigia kama utampata, na kama ukimpata huna hakika kama ubora wa mawasiliano utakua mzuri. Kila mahali watu wanapopiga simu wanalazimika kupayuka sauti ili kusikika, mara ukipiga simu unayempigia hapatikani hata kama mpo pamoja hapohapo (kama unajaribu), mara ukipiga simu unakutana na kelele za kuudhi.
 
Hii leo watanzania wanapotezewa muda, unapiga simu ili uongee na mtu fulani kwa haraka badala yake unapigiwa matangazo ya biashara kwanza kwa muda mrefu ndipo unajibiwa hapatikani ama unaunganishwa na muhusika.
 
Hii leo, watanzania wangapi wanaingiza vocha kwenye simu zinapotea, na ukifuatilia kwenye madawati ya wateja ya kampuni za simu hakuna msaada.
 
Hii leo makampuni ya simu yote madawati yake ya huduma kwa wateja ukipiga simu ya bure basi unapaswa utenge nusu saa kwa ajili ya kuuliza huduma Fulani ambayo kimsingi ni haki ya mteja na ya bure, tena makampuni mengine yameamua kuwabagua watanzania kuna huduma ya bure ya kusubiri hata saa nzima na kuna huduma ya kulipia.
 
Hii leo Serikali imetangaza kupungua kwa gharama za upigaji wa simu, nani kapunguza gharama hizo? badala yake watanzania wameanzishiwa utamaduni mpya wa kushiriki bahati nasibu ya kampuni za simu, mara tuma ujumbe ushinde milioni 50, nyumba nakadharika. Uhalali wa bahati nasibu hizi anaufuatilia nani, watanzania wanajua kinachofanyika kinaga ubaga?
 
Hii leo mawasiliano ya simu ya Kampuni Fulani yanaweza kukosekana hata siku nzima na watanzania hawaombwi radhi na hakuna fidia. 
 
Hii leo makampuni ya simu yanakusanya marundo ya faida na zote zinaishia kufanya matumizi ambayo hayana uangalizi kama huo uwajibikaji wa kijamii (Social Responsibility) una manufaa kwa watanzania? Hivi Kampuni ya simu kumleta msanii mkubwawa kimarekani na kumlipa mamilioni ya fedha ndio kipaumbele cha watanzania?
 
Yapo mengi yanayoudhi.
 
Mimi sina tatizo na maudhi ya makampuni haya ya simu kwa sababu najua kuwa makampuni haya yanatafuta faida.
 
Hoja yangu ni kwamba wanaofanywa vichwa vya wendawazimu ni watanzania. Kama ndivyo sie vyombo vya habari tumeshiriki vipi kulinyoosha hili?
 
Inawezekana nina majibu kuwa vyombo vyetu vya habari kwa sababu vinanufaika na matangazo ya biashara kutoka makampuni haya ndio maana haviwezi kuyakosea.
 
Sasa ninachojiuliza kwenye hili vipi wadau, tumeshindwa? tumetekwa na maadui? Bloggers msio na matangazo ya kampuni za simu, magazeti yasiyo na matangazo ya makampuni ya simu, Radio na Televisheni hapo vipi?
 
Watanzania wanaumia jamani, vibaya hivyo twende tuseme, hawa jamaa katika maeneo ambayo wapo makini nayo ni kulalamikiwa, wananchi wanalalamika lakini pa kulalamikia wanakosa kwa sababu sisi hatujawawezesha kulalamika. Vyombo vyetu vya habari ndio hivyo vinaogopa kunyea kambi.
 
Je tukae tu kimyaaaaa
 
Ahaaaaaa Jamani sio vizuri, tunakiuka weledi wetu, mbona  taasisi nyingine zikikosea tunaripoti lets do this please.
 
Kwa heriiiiiii
 
 



Siku nzuri niliyokutana na watu muhimu

 Nilipiga boksi na Kaka Zakaria Ngalimanayo, yeye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Klabu ya Wanalizombe Majimaji ya Songea ambayo ipo mawindoni kusaka kurejea Ligi kuu
 
Hapa nilikutana na Sheikh Jamal (Baba Mayasa) pili kulia, anayefuata ni Abdalah dege mmoja wa WanaCCM waliopata kuongoza Chama kwa heshima kubwa na baadaye akastaafu kistaarabu. Na kwanza Shoto ni Mpiganaji ninayemheshimu sana Juma Nyumayo Mwanataaluma mwenzangu.
 


Sunday, March 2, 2014

hufarijika kuwaona wapiganaji wakongwe



Mwandishi wa Habari Mkongwe hapa Nchini Mzee Mbunda wa kwanza kushoto, anafuatiwa na Andrew Kuchonjoma- Mwenyekiti Ruvuma Press Club, Andrew Chatwanga - Katibu Ruvuma Press Club, Nathan Mtega na Zakaria Nachoa - Mkurugenzi Manipsaa Songea
 
 Mpenda Mvula, Mmoja wa wapiganaji wakongwe katika mambo ya Uandishi wa Habari yeye akijikita katika upiga picha, waandishi wa habari wengi wakongwe hapa nchini wanamtambua huyu jamaa na mpaka leo angalia anatupiga jeki wadogo zake. Hongera sana Brother na Baba yetu katika fani, Big Respect



Samahani Wadau kwa kutoaga, sasa Nimerudi


Sunday, February 2, 2014

Mimi na Chama Cha Nani hii tumetimiza umri wa miaka 37.


 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akishangilia pamoja na wana CCM wa Manispaa ya Songea kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi). Mkutano huu ulifanyika katika uwanja wa Kibulang'oma kata ya Lizaboni, Songea Mjini katika Mkoa wa Ruvuma

 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akipongezana na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dr Emmanuel Nchimbi kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi)

 Wana CCM wakishangilia kwa nguvu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambacho sasa kimetimiza miaka 37 tangu kililetwa duniani mwaka 1977

 Mzee Mustafa Songambele mmoja wa waasisi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na mwanachama namba 15 wa Chama cha TANU akiwahusia wana CCM na wananchi wengine wa Songea

 Tunakushukuru Mzee Songambele kwa kutuanzishia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisikika akisema Mwigulu Nchemba. Anayewatazama nyuma ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho.

Dr Emmanuel Nchimbi, Kiongozi wa "Maneno kidogo, Kazi zaidi" akimwaga maelezo juu ya miradi lukuki ya maendeleo aliyowafanyia wananchi wa jimbo lake katika sekta ya Afya, Barabara, Usafi wa Mazingira, Michezo na Elimu. Jamaa alishangiliwa kuwa Jembe tena Jembe la Mpunga

 Mwigulu Nchemba akiwaaga wananchi wa Songea baada ya kuhunguruma katika Jukwaa la Miaka 37 ya tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, Mkutano uliohunguruma katika viwanja vya Kibulang'oma, Lizaboni Mjini Songea. Jamaa ajenda yake kuu ni Uzalendo na Utaifa kwa kila jambo na ndio maana muda wote ni skafu ya Bendera ya Taifa, I like this, Big respect Brother.


Friday, January 24, 2014

Hii imenikumbusha mbali sanaaaaaa

 Kijijini Ilembula, wilaya ya Wanging'ombe bado akina dogo wanalelewa kama ilivyokua mimi..


 Baada ya kumaliza kazi shambani safari ya nyumbani kuwahi ugali

Baba na mwana wakitoka kwenye majukumu.

Tuesday, January 21, 2014

Hongeraaaaa Mpiganaji Juma Nkamia


Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Juma Selemani Nkamia akipokewa na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Clement Mshana, katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Olegabriel

Hongera saaaaana Juma Nkamia.

Najua kwa pongezi hizi wapo ninaowaudhi lakini naomba wadau tujenge utamaduni wa kukubali mafanikio ya binadamu. 

Nampongeza Juma Seleman Nkamia, mwanahabari wa siku nyingi na mbaye pengine amekua kichocheo cha wana habari wengi wanaofanya vizuri hii leo kutokana na umahiri wake wa utangazaji.

Juma umetutoa kimasomaso, umetupa heshima unatuwakilisha. Sina mengi zaidi na sitaki kuzua mjadala naomba niikamilishe furaha yangu kwa kusema Cheza karata yako vizuri utusafishie njia sote tuliofurahi na wasiofurahi. Ukweli ni kwamba wewe ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Kwani kitu gani eheee, Kaji moja bana. Ahahahahaaaaa!!!!!