Sunday, February 2, 2014

Mimi na Chama Cha Nani hii tumetimiza umri wa miaka 37.


 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akishangilia pamoja na wana CCM wa Manispaa ya Songea kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi). Mkutano huu ulifanyika katika uwanja wa Kibulang'oma kata ya Lizaboni, Songea Mjini katika Mkoa wa Ruvuma

 Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akipongezana na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dr Emmanuel Nchimbi kwa Chama hicho kutimiza miaka 37 tangu kizaliwe mwaka 1977 (tulipozaliwa pamoja na mimi)

 Wana CCM wakishangilia kwa nguvu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi CCM ambacho sasa kimetimiza miaka 37 tangu kililetwa duniani mwaka 1977

 Mzee Mustafa Songambele mmoja wa waasisi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na mwanachama namba 15 wa Chama cha TANU akiwahusia wana CCM na wananchi wengine wa Songea

 Tunakushukuru Mzee Songambele kwa kutuanzishia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisikika akisema Mwigulu Nchemba. Anayewatazama nyuma ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho.

Dr Emmanuel Nchimbi, Kiongozi wa "Maneno kidogo, Kazi zaidi" akimwaga maelezo juu ya miradi lukuki ya maendeleo aliyowafanyia wananchi wa jimbo lake katika sekta ya Afya, Barabara, Usafi wa Mazingira, Michezo na Elimu. Jamaa alishangiliwa kuwa Jembe tena Jembe la Mpunga

 Mwigulu Nchemba akiwaaga wananchi wa Songea baada ya kuhunguruma katika Jukwaa la Miaka 37 ya tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, Mkutano uliohunguruma katika viwanja vya Kibulang'oma, Lizaboni Mjini Songea. Jamaa ajenda yake kuu ni Uzalendo na Utaifa kwa kila jambo na ndio maana muda wote ni skafu ya Bendera ya Taifa, I like this, Big respect Brother.