Friday, May 31, 2013

WABUNGE WA DRC WAMPONGEZA JK

IMG 7676 4d4b9
Kufuatia wito wa rais Jakaya Kikwete kwa marais wa mataifa ya maziwa Makuu marais Paul Kagame, wa Rwanda, Joseph Kabila wa jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Yoweri Museveni wa Uganda, kuzungumza na makundi ya waasi yanayopambana na nchi zao, wabunge wa Kongo Kwenye taarifa yao ya pamoja iliyosomwa na mbunge Benjamin Mukulungu , wabunge hao wa Kivu Kusini na Kaskazini wameomba kuwe na mtazamo wa jumla wa viongozi wa kanda ya maziwa makuu na umoja wa mataifa ili kumaliza vita nchini CongWabunge wa Kivu wamepongeza msimamo wa rais wa Tanzania Jakaya Kikwete wa kutaka kuwe na mazungumzo kati ya serikali za Congo Rwanda na Uganda na makundi ya waasi wanayopingana nayWabunge wa Kivu wametaka pendekezo la Rais Kikwete ni lazima lipewe kipaumbele na jumuiya ya kimataifa ili kuwe na amani ya kudumu kwenye eneo hilo.Mbunge wa upinzani Emerio Kunji kutoka jimbo la Kasai amesema amepanga kutoa hoja rasmi bungeni ili kuweko na azimio la bunge kuhusu msimamo ambao serikali ya Congo inatakiwa kuchukua kwa ajili ya kutatua mzozo wa Kivu

Mrehemu Ernest Zulu azikwa Maposeni Songea

Na Nathan Mtega,Songea
MWILI wa marehemu aliyekuwa mwandishi wa vikao vya Bunge la Tanzania Ernest Zulu umezikwa katika makaburi ya kichifu yaliyopo Maposeni Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma huku mazishi hayo yakifanyika bila kuhudhuriwa na familia yake jambo ambalo liliwashangaza baadhi ya watu waliohudhuria mazishi hayo.
  Wakiongea kwa sauti za chini kwenye mazishi hayo baadhi ya wakazi wa Peramiho walisema kuwa wameshangazwa kuona wasifu wa marehemu ukisomwa na kuonyesha kuwa marehemu amewaacha watoto wanne na mke mmoja lakini cha ajabu hawaonekani kwenye msiba huo.
      Kwa upande wake kaka wa marehemu  chifu Emmanuel Zulu akiwashukuru mamia ya watu walioshiriki kwenye mazishi hayo akiwemo akiwemo  Mbunge aliyetumwa na bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kuja kuwakilisha mazishi hayo Abdukalim Shaha wa jimbo la Mafia Zanzibar alisema kuwa yeye hana  cha zaidi ya kumshukuru Mungu aliyetenda mambo hayo.
      Aidha kwa upande wake Mbunge Abdukalim Shaha akitoa salaamu za bunge amewataka viongozi wa dini zote kuendelea kujenga mshikamano wa kuliombea taifa lisiingie kwenye machafuko maana amani ikitoweka hakuna atakayekuwa huru kwa kufanya kazi zake.
        Alisema kuwa marehemu Ernest Zulu alitokea katika familia ya kichifu lakini kafanya mambo mazuri mengi katika taifa kwa sababu wazazi wake walikuwa wakihimiza amani na utulivu vidumu siku zote na siyo vinginevyo hivyo jamii inapaswa kuiga na kuendeleza moyo huo wa uzalendo.
        Alisema kuwa hali ya sasa  inayojitokeza katika vikao vya bunge kwa baadhi ya viongozi kutaka kushikana mwilini hivyo ni vyema jamiin kwa ujumla ikasaidiana kumuomba Mungu aweze kuepusha balaa hasa kwa kuwakemea vijana waachane na ushabiki usiyokuwa wa msingi.
      Hata hivyo aliipongeza ofisi ya mkuu wa wilaya ya Songea kwa kazi nzuri ya kufanikisha maandalizi ya mazishi hayo kwa kuwapokea wageni na kufanikisha kuwapa huduma na kuwa hiyo wanaenda kuiweka kwenye rekodi ya ofisi ya Mbunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
    Lakini pamoja na wakazi hao kuhudhuria kwenye mazishi hayo wakiwemo viongozi wa safari ya mwisho ya Ernest Zulu lakini wananchi hao walionyeshwa kutoridhika kwa kutokuwepo Mbunge hata mmoja wa mkoani hapo zaidi ya wawakilishi.
VIA/ demashonews

Thursday, May 30, 2013

Kampuni ya usambazaji mbegu ya PANNAR SEED kanada ya kusini yatoa jezi 28 na mipira 5 kwa Timu za vijijini Songea


Meneja wa kanda ya kusini Torio Mafie toka kushoto kwako akiwa ameshikilia mpira pamoja na jezi wakati akimuonyesha mkuu wa wilaya ya Songea jana ofini kwake.
............................................
Hii ni baaada ya kukamilika kwa msimu wa mavuno kwa wakulima wa wilaya ya SONGEA mkoani RUVUMA sasa kampuni ya usambazaji mbegu ya PANNAR SEED kanda ya nyanda za juu kusini imetoa vifaa vya michezo wa soka kwa wakulima ili kufufua michezo wakati wakiwa waanajiandaa kwa msimu mwingine wa kilimo.

Kampuni ya PANNAR SEED imetoa jezi 28 na mipira mitano vyenye thamani ya shilingi milioni 2 na laki moja ambapo MENEJA WA KANDA YA KUSINI TORIO MAFIE amesema msaada huo waliotoa ni ishara kuwa wapo pamoja na wakulima ili kuwapa vijana shughuli mbadala wakati wa mapumziko ya msimu wa kilimo
Mkuu wa wilaya ya SONGEA JOSEPH MKIRIKITI Akipokea  jezi na mipira kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya
PANNAR SEED
Mkuu wa wilaya ya SONGEA JOSEPH MKIRIKITI akitabasamu kwa furaha baada ya wakulima kuwezeshwa vifaa vya michezo ,
 Hataa hivyo kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya SONGEA amesema bado mahitaji ya vifaa vya michezo ni makubwa hivyo ameziomba kampuni mbalimbali zinazojihusisha na shughuli za kiuchumi na kijamii wajitokeze kufadhiri timu za vijiji wilayani hapa

SIKU YA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA KUMI NA SABA(17) YA WIKI YA MAZIWA SONGEA-RUVUMA YAFANA



Mkuu wa mkoa wa RUVUMA SAID MWAMBUNGU amezindua maadhimisho ya 17 ya wiki ya maziwa nchini na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuwa na utamaduni wa kunywa maziwa kwa wingi kwa lengo la kuboresha afya zao

Akizungumza na wananchi na wadau wa maziwa katika viwanja vya manispaa ya SONGEA MWAMBUNGU alisema  kati ya lita bilioni 1.6 za maziwa zinazozalishwa hapa nchi kwa mwaka ni wastani wa lita 11.6 tu zinazonywewa na mtu mmoja wa mkoa wa Ruvuma kiasi ambacho ni kidogo ukilinganisha na viwango vya kimataifa vya lita 200 kwa mtu kwa mwaka.
Maadimisho hayo ya wiki ya maziwa ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza mkoaniMkoani Ruvuma ambapo MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU aliwaamasisha wananchi wa mkoa wake kuongeza kasi ya unywaji wa maziwa sambamba na kufuga ng’ombe wa kisasa wanaotoa maziwa mengi badala ya ng’ombe wa asili ambao uzalishaji wao ni mdogo.

Maadhimisho haya yameambatana na maonyesho ya bidhaa mbalimbali za maziwa pamoja utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa unywaji maziwa, usindikaji na uzalishaji wake hata hivyo baadhi ya wadau wa maziwa kutoka vyama vya usindikaji maziwa wamesema maziwa mengi yanayozalishwa hapa nchini yanashindwa kuwafikia wanywaji kutokana na asilimia chache zinazosindikwa.
Wiki ya maziwa iliyozinduliwa leo mkoani hapa itaendelea kwa siku nne zijazo ambapo hapo kesho madereva wa pikipiki maarufu kama YEBOYEBO, wafungwa na wagonjwa hospitalini watagawiwa maziwa ya bure kama sehemu ya uhamasishaji


Tuesday, May 28, 2013

Kinana: Akemea wanaowania urais 2015

kinana 3361e
Kinana (katikati)
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana amesisitiza kwamba Chama kitamwadhibu bila huruma mwanachama yeyote anayejipitisha-pitisha katika maeneo mbalimbali na kufanya kampeni za kuwania urais kabla ya wakati.

Kinana alisema hayo jana wakati akizungumza na Kamati ya Siasa na mkoa wa Iringa, katika kikao maalum, kilichofanyika kabla  ya kwenda mkoani Njombe ambako ameanza ziara ya siku saba mkoani humo.

Kinana alisema, katazo la wanachama kujipitisha-pitisha na kupiga kampeni za kuwania urais au nafasi yoyote kabla ya muda  halitoki midomoni mwa viongozi bali ni kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama.

"Ndugu zanguni, nawakumbusha kwamba kwa hili hatuna mzaha nalo, hivyo hakikisheni kila mmoja wenu kama kiongozi hajihusishi kwa namna yoyote kushiriki katika kutumiwa na wanachama hao wanaojipitishajiptisha", alisema Kinana na kuongeza;
"Ni lazima Chama kiwe kikali kwenye jambo hili, kwa sababu kama kitawaacha watu hawa kukiuka taratibu na kanunzi za Chama wanazidi kukifanya chama kuwa na makundi mengi ambayo yatakipeleka pabaya," alisema Kinana

Kinana alisema,  kazi walioyonayo wale wote wanaokitakia mema Chama, ni kumuunga mkono Mwenyekiti, Rais Jakaya katika kazi ya kuhakikisha CCM inakamilisha utekelezaji ilani yake ya Uchaguzi kwa kiwango kinachostahili na siyo muda kujipitisha pitisha mtu binaafsi kwa wanachama huku utekelezaji wa ilani ukisinzia.

Alisema kuwa hivi sasa kazi ya CCM ni kuhakikisha inatekeleza ilani ya uchaguzi kwa kipindi kilichobaki cha miaka miwili ya nusu kabla ya kumalizi kwa awamu ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete.
"Ni wazi kazi yatu CCM ni kuhakikisha tunatekeleza ilani ya uchaguzi kwa vitendo na si mamneno kama wanavyofanya wengine. ni kazi kubwa imefanyika chini ya uongozi wa Rais Kikwete na katika kipindi cha miaka miwili iliyobaki tumedhamiria kuifanya zaidi", 

Alisema moja ya maeneo ambayo licha ya kuwepo changamoto za hapa na pele lakini yamefanikisha sana utekelezaji wa ilani ya CCM,  ni kwenye Halmashauri mbalimbali nchini ambapo watendaji walio wengi wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi.

"Kwa kweli CCM lazima hawa tuwapongeze maana kuna wengine kazi yao imebaki kuwashambulia huku wakijua watendaji hao hawana fursa ya kujitete mbele ya jamii. chapeni kazi nasi tupo nyuma yenu, na kila wakati tutakuwa tukitambua juhudi na kazi kubwa mnayoifanya kwa jamii," alisema Kinana. 

Chanzo: Bashir Nkoromo

Mama aliyejifungua watoto watano aruhusiwa kutoka hospitali baada ya kuomba

Bi Sophia Mgaya aliyekaa kitandani akiwa amebeba mmoja wa  wawatoto watano aliowazaa kabla ya watototo hao kufa wote(Picha na maktaba)
Hawa ndio watoto aliojifungua katika hospital ya Mkoa wa Ruvuma na kesho wakafaliki dunia (Picha na maktaba)
..........................................................................
Na Nathan Mtega,Songea
 MWALIMU Sophia Mgaya(28) mkazi wa Ruhuwiko mjini Songea mkoani Ruvuma aliyejifungua watoto watano kwa wakati mmoja kwa njia ya upasuaji mnamo Mei 25 mwaka huu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma iliyopo mjini Songea na watoto hao kuishi kwa muda wa masaa kumi kabla hawajafariki dunia ameruhusiwa kutoka hospitalini hapo.

Akizungumza na Demashonews kwa njia ya simu Sophia Mgaya akiwa nyumbani kwake Ruhuwiko mjini Songea alisema alilazimika kuomba kutoka wodini kwa sababu alikuwa akijisikia uchungu anapowaona wanawake wenzake wodini humo wakiwakumbatia watoto wao baada ya kujifungua huku wa kwake wote wakiwa wamefariki dunia baada ya kuzaliwa. 

Alisema kuwa muda wote aliokuwa hospitalini hapo baada ya watoto wake kufariki huku akiwa bado anauguza kidonda cha upasuaji aliofanyiwa alikuwa akilia muda wote anapowaona wanawake wenzake waliojifungua wakiwakumbatia na kuwanyonyesha watoto wao hivyo akaamua kuomba aruhusiwe kutoka hospitalini hapo. 

 ‘’Niliomba kuruhusiwa kutoka hospitali na kwenda kujiuguza kidonda nyumbani kwa sababu ya uchungu na majonzi niiiyokuwa nikiyapata wodini hapo ninapowaona wanawake wenzangu waliojifungua wakiwakumbatia na kuwanyonyesha watoto wao huku wa kwangu wakiwa wameshazikwa”alisema Bi.Mgaya 

Aidha aliushukuru uongozi wa hospitali hiyo pamoja na wafanyakazi wote kwa namna walivyomuhudumia yeye pamoja na watoto wake watano waliozaliwa na kuishi kwa muda wa masaa ya kumi ambapo alisema kuwa yote yaliyotokea anaamini kuwa ni mapenzi ya Mungu.

Mganga Mkuu mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma Dkt.Benedict Ngaiza akizungumza na mwandishi wetu  kwa njia ya simu kuwa waliamua kuridhia ombi la mama huyo kuondoka hospitalini hapo baada ya kujiridhisha kuwa anaendelea vizuri kwa sababu walifanya kila walichoweza kukoa uhai wake na watoto lakini watoto walifariki baada ya masaa kumi. 

Wakizungumza baadhi ya wananchi waliomshuhudia mama huyo na watoto wake baada ya kuzaliwa na  kabla hawajafariki walisema kuwa kuna kila sababu kwa kila mwenye uwezo wa kumsaidia mama huyo kwa namna yoyote afanye hivyo
Bi.Marietha Ngonyani na Lusi Haule wakazi wa mjini Songea waliwaomba wananchi mbali mbali kujitolea kumsaidia mama huyo kwa sababu bado anauguza kidonda cha upasuaji aliofanyiwa na pia tukio hilo limemuathiri kisaikolojia pia hivyo anahitaji faraja. 
 
VIA/ www.demashonews.blogspot.com

RAIS DKT. KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI MBALIMBALI ADDIS ABABA, ETHIOPIA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Mohamed Morsi walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Mohamed Morsi walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) professor Ntumba Luaba na ujumbe wake  walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia ad15 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia
  ad16 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia ad17 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza  Waziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia
  ad18 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulishaWaziri Mkuu wa  Jamaica Bi. Portia Simpson Miller kwa Mhe Gideon Moi, Seneta wa Kaunti ya Baringo nchini kenya na ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha KANU cha nchi hiyo walipokutana pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU)  jijini Addis Ababa, Ethiopia
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani Mh Liberata Mulamula walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU)  jijini Addis Ababa, Ethiopia g3 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa taaisi ya kimataifa inayoshughulikia mapambano dhidi ya Ukimwei, Kifua Kikuu na Malaria ya The Global Fund Dkt Mark Dybil  na afisa wa taasisi hiyo Bi Shu-shu Tekle-Haimanot walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia  IMG_7116 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha kwa mazungumzo  Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibe walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia
IMG_7134 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibe pamoja na Mratibu wa Masuala ya Ukimwi wa Marekani Balozi Eric Goosby walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya  mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia

WADAU JITOKEZENI KUDHAMINI UHURU MARATHON!!

2 
Katibu mkuu wa Chama Cha Riadha Tanzania, Seleman Nyambui akiongea katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa wadhamini wa Uhuru Marathon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Pembeni ni mkurugenzi wa Kampuni ya Intellectuals ambao ndiyo waandaaji wa mbio hizo, Innocent Melleck.
 4 MKurugenzi wa Kampuni ya Intellectuals ambao ndiyo waandaaji wa mbio hizo, Innocent Melleck akiongea katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa wadhamini wa Uhuru Marathon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Katibu mkuu wa Chama Cha Riadha Tanzania, Seleman Nyambui. 3 
Waandishi wa Habari waliohudhuria mkutano huo wakiwajibika  wakati wa ufunguzi wa wadhamini wa Uhuru Marathon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu
WAKATI mbio zinazosubiriwa kwa hamu kubwa na watu wengi hapa nchini za Uhuru Marathon zikitarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu, waratibu wa mbio hizo wamezitaka kampuni, taasisi au watu binafasi wanaotaka kuzidhamini wafanye hivyo.
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Intellectuals walio waandaaji wa mbio hizo, Innocent Melleck alisema wameamua kufungua milango ya udhamini, ili ziweze kufana zaidi.
 Melleck alisema, wanariadha wengi kutoka ndani na nje ya nchi wameonyesha nia ya kushiriki mbio hizo zitakazokuwa zikifanyika kila Desemba zikiambatana na maadhimisho ya sherehe za uhuru wa Tanzania Bara, hivyo wameona ni bora wafungue milango kwa wadhamini.
 “Nadhani wote mnakumbuka uzinduzi wa mbio hizi za Uhuru, uliofanyika Desemba mwaka Jana, ukiwa unaashiria kuanza kwa mchakato wa maandalizi ya mbio zenyewe ambazo zitaanza kufanyika Desemba mwaka huu.
“Mbio hizi za Uhuru, kama lilivyo jina lake zimeanzishwa ili kuongeza chachu kwa Watanzania kuwa na moyo wa kulinda amani, umoja na mshikamano wetu.
 “Kwa sasa maandalizi ya awali yanaendelea vizuri, nasi tumeona huu ni muda muafaka kufungua milango ya udhamini kwa makampuni, mashirika na taasisi mbalimbali ambazo zitahitaji kushirikiana nasi katika kufanikisha mbio hizi wajitokeze na kupata taratibu za udhamini,” alisema Melleck.
 Alisema kutakuwa na mbio ndefu za kilomita 42, mbio za kati za kilomita 21 na zile za kujifurahisha za kilomita 5, hivyo mdhamini anaweza kuchagua aina ya mbio anazotaka kuzidhamini.
 Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT), Suleiman Nyambui alisema, tayari kwa upande wao wamekamilisha vitu vingi ikiwemo kupendekeza mzunguko wa mbio hizo na kuangalia mambo yote ya kiufundi.
 “Tunawaomba wadhamini wajitokeze ili kwa pamoja tuweze kufanikisha mbio hizi zenye malengo mazuri kwa Taifa letu kwa ujumla. 
 “Mbio hizi tutazisimamia na kuziendesha katika hadhi ya kimataifa ili kuhakikisha kuwa zaidi ya kulinda Amani na Umoja wetu, pia tunalitangaza taifa letu kote ulimwenguni.
 “Kwa kuwa mimi ninaangalia zaidi upande wa ufundi, nichukue nafasi hii pia kuwasihi wanariadha wa hapa nchini kuanza maandalizi ya mbio hizi, itakuwa si vyema nafasi za juu zikichukuliwa na wageni, wakati sisi tunao wanariadha wazuri hapa nyumbani,” alisema.
Uhuru Marathon ni moja kati ya mbio zinazotarajiwa kuleta mapinduzi mapya katika riadha, ikiwa pamoja na kukumbusha umuhimu wa kutunza na kulinda amani tuliyonayo.

Taswira Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa:Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe Ashiriki Maandamano ya kuadhimisha miaka 50 OAU/AU Jijini Dar es Salaam Nakusema :'' Umoja wa Afrika (OAU/AU) umepata mafanikio makubwa tangu kuanzishwa kwake mjini Addis Ababa, Ethiopia tarehe 25 Mei, 1963''.

"Brass Band" ikiongoza maandamano kutokea Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuelekea Viwanja vya Karimjee kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50 OAU/AU.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akimkabidhi Mkuu wa Mabalozi na Balozi wa DRC hapa nchini, Mhe. Juma Khalfan Mpango Mwenge wa Umoja wa Afrika (OAU/AU) kuashiria kuanza kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja huo yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam
 Picha zaidi za maandamano.
 Mhe. Membe akishiriki maandamano hayo.
Mhe. Membe, Mabalozi, wananchi na wageni waalikwa wakiwa katika maandamano hayo kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika
 Mhe. Membe akisikiliza Wimbo wa Taifa na AU zilizopigwa kuadhimisha miaka 50 ya umoja huo
 Picha zaidi wakati wa wimbo wa Taifa
  Mhe. Membe, Mabalozi, na Viongozi wengine  wakiangalia burudani kutoka vikundi mbalimbali vya utamaduni vilivyopamba maadhimisho hayo
 Burudani ikiendelea.
Kikundi kingine cha burudani kilichopamba sherehe hizo.Picha Zote na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
--
Na Ally Kondo
Umoja wa Afrika (OAU/AU) umepata mafanikio makubwa tangu kuanzishwa kwake mjini Addis Ababa, Ethiopia tarehe 25 Mei, 1963.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) katika sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja huo iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam tarehe 25 Mei, 2013.

Mhe. Membe alieleza kuwa, AU imefanikiwa kutimiza lengo la kuzikomboa nchi zote za Bara la Afrika isipokuwa Saharawi kutoka katika tawala za kikoloni. Alisema katika kufanikisha hilo, Tanzania imechangia kwa kiasi kikubwa kwani, Makao Makuu ya Ukombozi ya AU yalikuwa hapa nchini.

Kuhusu Demokrasia na Utawala Bora katika nchi za Afrika, Mhe. Waziri alisema kuwa AU imeweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kuwa wanachama wake wanaheshimu utawala wa sheria kwa kuweka sheria kali za kukomesha tabia ya kuingia madarakani kwa njia ya mapinduzi ya kijeshi. Sheria hizo ni pamoja na; nchi inayotawaliwa kijeshi kusimamishwa uanachama wa AU, kuwekewa vikwazo vya kiuchumi pamoja na Kiongozi wa Mapinduzi kutoruhusiwa kuwania nafasi ya Urais katika uchaguzi wa kidemokrasia.

Kutokana na msimamo huo, AU imefanikiwa kupunguza matukio ya mapinduzi katika nchi za Afrika tangu ilipoanzishwa. “Afrika imeshuhudia matukio ya mapinduzi matano katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ukilinganisha na matukio 34 yaliyotokea kabla ya kipindi hicho”. Mhe. Membe alisikika akisema.

Katika kukabiliana na migogoro inayozuka mara kwa mara katika nchi za Afrika, alisema kuwa, AU imebadilisha kipengele ambacho kilikuwa kinakataza nchi za Afrika kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine. Hivyo, kutokana na mabadiliko hayo nchi za Afrika sasa zinaweza kuingia katika nchi nyingine kulinda amani.

Kwa upande wa maendeleo ya kiuchumi, Mhe. Waziri alisema kuwa hatua kubwa imefikiwa, hususan kupitia Jumuiya za Kiuchumi za Kikanda, kama vile SADC, EAC na ECOWAS. Hata hivyo alibainisha kuwa, ukosefu wa miundombinu imara kama barabra na reli, kuunganisha Bara zima la Afrika ni kikwazo katika kufikia malengo ya kiuchumi kwa nchi nyingi za Afrika.

Sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (OAU/AU) zilipambwa na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasha mwenge wa AU, maandamano na burudani kutoka vikundi mbalimbali vya utamaduni. Aidha, sherehe hizo zilihudhuriwa na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimatafa hapa nchini, wanafunzi na wananchi.

Monday, May 27, 2013

BREAKING NEWS: WATU NANE WAFALIKI DUNIA NA WENGINE KUMI NA MOJA MAJELUHI KATIKA AJALI YA GARI - NAMTUMBO

Hili ndilo lori lililopata ajali katika kijiji cha Hanga
..............................................
Watu nane wamefariki dunia  baada ya gari walilokuwa wanasafiria kutoka kijiji cha mputa wilaya ya Namtumbo kwenda Songea  kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Hanga eneo la Bombambili wilaya ya Namtumbo mkoa wa Ruvuma .
Roli hilo lilikuwa limebeba magunia ya ufuta, mpunga wakiwemo na abiria

 Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma  Deusdedit  Nsimeki amesema ajali hiyo imetokea jana Tarehe 26.05.2013 majira ya saa nne na nusu( 4:30 usiku  katika kijiji cha Hanga eneo la bombambili mkoa wa Ruvuma, chanzo cha ajili hiyo ni mwendokasi na dereva kuendesha gari akiwa amelewa,

Ajali hiyo  imehusisha gari lenye namba za usajili T.677 ADL  aina ya Isuzu lori , mali ya mfanyabiashara wa mazao maarufu kwa jina la Mtazamo. likiendeshwa na dereva aitwae CHRISTIN NYONI mwenye umri wa miaka 30, mkazi wa LIHULI SONGEA,
Baada ya ajali hiyo kutokea dereva wa gari hilo amekimbia na kutelekeza gari porini hadi sasa jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linafanya jitihada za kumtafuta ili sheria ifuate mkondo wake.

Kamanda wa Polisi amesema gari  hilo liliacha njia baada ya kugonga daraja na kupinduka na kusababisha vifo vya watu nane(8)  na majeruhi kumi na moja (11) ambao
wote wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kwa matibabu.

Kutokana  na ajali hiyo mbaya kamanda wa polisi wa  Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki ametoa wito kwa wamiliki wa magari ya mizigo kutopakia mazao pamoja na abiria na atakayekiuka atachukiliwa hatua kali za kisheria.
Pia ametoa wito kwa wamiliki/wasimamizi wa magari kuwa wanatakiwa kuhakikisha magari ya mizigo,mazao hayapakii abiria na atakaye kiuka agizo hili hatafikishwa mahakamani mala moja 
ambapo


Sunday, May 26, 2013

Dr Hosea tunakusalimia!!!!

Wadau leo nimejisikia tu kumsalimia Dr Hosea wa TAKUKURU. 
Kama nimewayeyusha sorry!!!

Huu ni Msimu wa viazi vitamu Songea. Rambo moja buku mbili tuuuuuuuu!!!!!!!

Kandokando mwa barabara kuu ya Songea kwenda Njombe Vijiji vya Mtyangimbole, Hanga, Mlilayoyo hadi Madaba, Viazi vitamu kibao, buku zako mbili unabeba rambo nzima ya viazi. Songea maisha tambalale!!!!!

Vitamu hivyo balaaaaaaaa!!!!

Akina dada hujipatia ajira wakati huu ya kuuza viazi kandokando mwa Barabara

Leta buku mbili nikuachie