Saturday, June 29, 2013

KESHO NDIYO KESHO KWA TIMU YA MAJI MAJI - SONGEA

 Timu ya Maji Maji songea kesho inaingia katika kinyang'anyilo cha uchaguzi wa viongozi huyo hapo ni Humphery Millanzi mgombea nafasi ya mwekiti katika timu ya Maji Maji akimwaga sela zake leo katika mdahalo uliofanyika leo hii jioni majira ya saa kumi katika Radio Jogoo kwa kushirikiana na Demashonews.blogspot.com, Moja ya ahadi zake ni kuhakikisha timu ya Maji Maji inapanda daraja , kuhakikisha timu inakuwa na wanachama hai na wakudumu kwa kuandaa mikutanao na kunadi sela za timu pia kuisaidia timu inakuwa na vyanzo vya pesa ili timu kuondokana na omba omba vile vile timu kuwa kampuni. Ameendelea kusema kwa kipindi hiki akiwa kiongozi wa mpito ameweza kuisaidia timu hadi kushika nafasi ya pili wakati timu haina vyanzo vya mapato hivyo sasa atakuwa na tiba mbadala katika kuiwezesha timu hiyo endapo atachaguliwa.
Toka kushoto ni Shekhan Mzaina akiwa na Hilda Kapinga mgombea nafasi ya ujumbe pia ni mmiliki wa timu ya Luwiko football Academy ya watoto chini ya miaka kumi na saba ana aihidi kuifikisha timu ya Maji Maji mbali sana akiwa kama mpenzi wa mpira wa miguu , huku akitolea mfano wakati timu hiyo ilipoenda kucheza Mbeya na kufungwa bao 6 kutokana na wachezaji  kutokuwa na uwezo wa kifedha na kuwa na mazingira mabovu
 Toka kulia kwako ni Salum Masamaki, Said Mangwe wagombea nafasi ya wajumbe na Mohamedi Issa mgombea nafasi ya Mwenyekiti.
 Toka kushoto ni Mohamed Mtika mgombea nafasi ya ujumbe akiwa na Hamphery Millanzi mgombea nafasi ya mwenyekiti wakitafakali kwa kina juu ya sela za wenzao walizokuwa wakitoa katika mdahalo uliokuwa ukiendelea katika Studio za jogoo FM kwa kushirikiana na demashonews.blogspot.com
 Toka kushoto ni Mohamed Mtika mgombea nafasi ya wajumbe , Hamphery Millanzi mgombea nafasi ya mwenyekiti, John Kabisana mgombea nafasi ya wajumbe na Mohamed Issa mgombea nafasi ya mwenyekiti

Toka kushoto ni mtangazi wa Radio Jogoo kipindi cha michezo Hosam Ulaya , Shekhan Mzaina na Hilda Kapinga mgombea nafasi ya wajumbe
 Wagombea uongozi katika Timu ya Maji Maji wakiandika maswali yaliyokuwa yakiuliuzwa kwa njia ya simu na wasikilizaji kupitia Radio Jogoo
 Baada ya kutoka katika mdahalo
 Picha ya pamoja toka kulia walio simama ni Hamphery Millanzi mgombea nafasi ya mwenyekiti,Said Mangwe wagombea nafasi ya wajumbe,Mohamed Issa mgombea nafasi ya mwenyekiti, Mchele, Tamimu Adamu  mtangazaji wa Radio Jogoo,Mohamed Mtika mgombea nafasi ya wajumbe,Salum Masamaki, John Kabisana mgombea nafasi ya wajumbe na kuoka kulia kwa walio chuchumaa ni Hilda Kapinga mgombe nafasi ya wajumbe, Shekhan Mzaina  na Hosam Ulaya
Humphery Millanzi mgombea nafasi ya mwekiti akiteta jambo na Hilda Kapiga mgombea nafasi ya wajumbe.
Kesho ndiyo siku ambayo itakwenda kuandika historia mpya katika timu ya Maji Maji kwa kufanyika uchaguzi kuanzia saa  saa nne asubuhi na leo ilikuwa ni kujinadi kila mgombea kutoa sera zake mambo yote kesho

Thursday, June 27, 2013

Tangazo Muhimu kutoka Wizara ya Afya

 

TAARIFA KWA MADAKTARI ,WAFAMASIA , MAAFISA AFYA MAZINGIRA NA MAAFISA WATEKNOLOJIA MAABARA WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI WAKIWA BADO WAKO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO (INTERNSHIP).

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapenda kuwataarifu waajiri wote kwamba, katika zoezi la upangaji wa vituo vya kazi imebainika kwamba kwa bahati mbaya wamepangwa madaktari ,wafamasia , maafisa afya mazingira na maafisa wateknolojia maabara ambao bado wako kwenye mafunzo kwa vitendo (internship).

Madaktari ,wafamasia , maafisa afya mazingira na maafisa wateknolojia maabara hawa, hawajasajiliwa kwenye mabaraza yao ya kitaaluma ikiwa ni moja ya masharti wanayotakiwa kutimiza kabla ya kuajiriwa Serikalini kwa mujibu wa Waraka wa Utumishi Na.1 wa mwaka 2009, kuhusu miundo ya kada zilizo chini ya Wizara ya Afya na ustawi wa Jamii. Kwa taarifa hii, wahusika wameondolewa kwenye orodha ya waliopangiwa kazi na nafasi zao zitajazwa na wataalam wengine wenye sifa kwa mujibu wa Muundo.

Aidha, kwa tangazo hili, tunapenda kusisitiza kwamba kwa wale wote waliopangiwa vituo vya kazi wakaripoti moja kwa moja kwa mamlaka ya ajira zao wakiwa na vyeti vya kumaliza mafunzo kwa vitendo (Internship),usajili wa muda(MD), usajili wa kudumu(DDS) na wafamasia.Hakutakuwepo barua maalum za kuwatambulisha kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, hivyo waajiri wote wanatakiwa kuwapokea na kuwapangia kazi.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza na utakaojitokeza kwa waajiri pamoja na wataalam waliopangiwa vituo kwa makosa.

Orodha ya wataalam waliopangiwa vituo vya kazi kwa makosa ni kama ifuatavyo:

         MADAKTARI WALIO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO NA AMBAO HAWAJASALIWA
        JINA    JINSI   ANUANI  KITUO CHA KAZI
1       DR. ADROSTER METHOD KYAKABANJA  KE      C/O SEKOU TOURE REG. HOSP. S.L.P. 132, MWANZA   MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA KYERWA
2       DR. CASTORY J. MWANGA   ME      S.L.P. 1470 MOSHI       KATIBU TAWALA MKOA WA  MTWARA
3       DR. CHRISTIAN MICHAEL   ME      SLP 65007, DSM. MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MAKAMBAKO
4       DR. DANSTAN NGENZI      ME      S.L.P. 8, IRINGA        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MULEBA
5       DR. DAVID MWASOTA       ME      S.L.P. 1483, MBEYA      KATIBU TAWALA MKOA WA  SINGIDA
6       DR. ENOCK F. MOYO       ME      SLP 82, SONGEA. MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA SIMANJIRO
7       DR. ESTHER TIMOTH       KE      SLP 9083 DSM    KATIBU TAWALA MKOA WA ARUSHA
8       DR. FAUSTINA E. MBUYA   KE      SLP 2946, DSM.  KATIBU TAWALA MKOA WA  LINDI
9       DR. FEISAL  A. SAID     KE      10773 DSM       MKURUGENZI WA JIJI TANGA
10      DR. FELICIAN KACHINDE   ME      S.L.P. 2289, DSM        MKURUGENZI WA MANISPAA YA KIGOMA
11      DR. FRIDA PASCAL NJAU   KE      SLP 11535, ARUSHA.      MKURUGENZI WA MANISPAA YA ARUSHA
12      DR. FURAHA MWAKAFWILA   ME      SLP 29, TUNDUMA.        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA KILOLO
13      DR. GABRIEL CHAMBALO    ME      C/O JUMA M. MAKUNGUS.L.P. 25, MEATU     MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MEATU
14      DR. GENDAGENDA MKOMBOZI ME      SLP 65014, DSM. MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA SERENGETI
15      DR. GORDIAN J. KIKOMPOLISI      ME      S.L.P. 65007, DSM       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MISENYI
16      DR. HALID GONGORO       ME              MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA BAGAMOYO
17      DR. HAMIDU ADINANI      ME      S.L.P. 1438, MOSHI      KATIBU TAWALA MKOA WA  SIMIYU
18      DR. HENRICK B. MAHENGE  ME      S.L.P 1446 IRINGA       KATIBU TAWALA MKOA WA  KILIMANJARO
19      DR. HENRY CHINYUKA      ME      C/O GOOD SAMARTAN OF TZ S.L.P. 3010 MOSHI       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA ULANGA
20      DR. HENRY JACKSON       ME              KATIBU TAWALA MKOA WA  SINGIDA
21      DR. HONSIA ELISA MOSHI  ME      S.L.P. 419, MBEYA       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA SIKONGE
22      DR. IMMACULATE HENRY KALUNGI    KE      SLP 65471, DSM. KATIBU TAWALA MKOA WA  RUKWA
23      DR. JAIROS N. HILIZA    ME      C/O MULERA PARISH, SLP 71, KASULU.      MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA UVINZA
24      DR. JANE KAGOLI MAGANGA KE      SLP 10255, MWANZA.      KATIBU TAWALA MKOA WA  KAGERA
25      DR. JOHN LUHAGA ME      S L P 1464, BUGANDO     MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MISUNGWI
26      DR. LEE M. MWAKALINGA   ME      S.L.P. 3888, MBEYA      MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA RUNGWE
27      DR. MAJA LUKANYA SOSOMA ME      S.L.P. 361, BARIADI - SIMIYU    MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA BUKOMBE
28      DR. MAJALIWA GERALD MARWA       ME              KATIBU TAWALA MKOA WA  KILIMANJARO
29      DR. MANYANZA SYLVESTER MPONEJA  ME      S.L.P. 31891, DSM       KATIBU TAWALA MKOA WA  NJOMBE
30      DR. MARIA E. KAPINGA    KE      SLP 5628 DSM    MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA UVINZA
31      DR. MHANDO JOHN ME      S.L.P. 904, DODOMA      KATIBU TAWALA MKOA WA  MOROGORO
32      DR. MUSSA GABRIEL       ME      SLP 419 MBEYA   KATIBU TAWALA MKOA WA  NJOMBE
33      DR. NASSIB DAUD MSUYA   ME      SLP 419, MBEYA. MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA NZEGA
34      DR. NIKUNDIWE KAJIRU    ME      S.L.P. 419, MBEYA       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA KYELA
35      DR. NTUGWA NYOROBI      ME      S.L.P. 1, MASWA SIMIYU  KATIBU TAWALA MKOA WA  SIMIYU
36      DR. NURU NDOMONDO       KE              KATIBU TAWALA MKOA WA  KAGERA
37      DR. RAJABU A. MRAMBA    ME      SLP 11501, DSM. KATIBU MKUU WAIZARA YA FYA NA USTAWI JAMII (MBEYA RUFAA)
38      DR. SAMWEL C. MKUMBE    ME      SLP 2923, MBEYA.        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA HANDENI
39      DR. SHEEL AHMED SALEEM  ME      S.L.P. 40552, DSM       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA LINDI
40      DR. SOPHIA VALERIAN MOSHA       KE      SLP 132, MWANZA.        KATIBU TAWALA MKOA WA  KAGERA
41      DR. SUKE  KUBITA MAGEMBE        ME      SLP 132, MWANZA.        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA KWIMBA
42      DR. WBESTER CHAMI       ME      S.L.P 152 S'WANGA       KATIBU MKUU WAIZARA YA FYA NA USTAWI JAMII (SUMBAWANGA CATC)
43      DR. WILLIAM BENEDICT KAIJAGE    ME      SLP 33, KALIUA. KATIBU TAWALA MKOA WA  TABORA
44      DR. ZAWADI BWANALI      ME      S.L.P. 634, MASASI      KATIBU TAWALA MKOA WA MTWARA
45      DR. ZENA A. SULEIMAN    KE      S.L.P 72735 DSM KATIBU TAWALA MKOA WA  SIMIYU


WAFAMASIA WALIO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO (INTERNSHIP)
        JINA    JINSI   ANUANI  KITUO CHA KAZI/MWAJIRI
1       ANOLD KATIKIRO  ME      S.L.P 419 MBEYA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MASWA
2       APOLINARY MWAKABANA     ME      S.L.P 170 IPINDA - KYELA        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MOMBA
3       ERIC MUHIKAMBELE        ME      S.L.P 5472 MOROGORO     KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA
4       EULAMBIUS MATHIAS       ME      S.L.P.267, LUSHOTO      MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA LUSHOTO
5       KALENDOLO J. MASATU     ME              MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE
6       MAGEMBE K. NGASSA       ME      S.L.P.100, SAME KATIBU MKUU WIZRA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
7       MARTIN JACKSON  ME      S L P 87, ARUSHA        KATIBU TAWALA MKOA WA MARA
8       MOHAMED S. ULOMBE       ME      S.L.P 31791 DSM MKURUGENZI WA MANISPAA YA MTWARA
9       MUSTAPHA LUTAVI ME      S L P24258, DAR ES SALAAM       MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA HANDENI
10      OSWALD MWIHAVA  ME      S.L.P 19374 DSM KATIBU TAWALA MKOA WA LINDI
11      SYLIVIA S. SWAI KE      S LP 860, BUKOBA        MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA BUKOBA
12      THERESIA  E. SHEMSIKA   KE      S.L.P.3054, MOSHI       KATIBU MKUU WIZRA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
13      TIMOTHEO SAMWEL ME      S.L.P 419 MBEYA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MLELE
14      CHIMPAYE JULIUS ME      S.L.P 12654 DSM MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA RORYA
15      KENETH JOHN     ME      S.L.P 154  MANYONI SINGIDA      MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA BUKOMBE
16      MASUDI LUGANDYA ME      S.L.P 1370 MWANZA       MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI MASASI
17      RENATUS FRANCIS ME      S.L.P 44 MWANZA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA NAMTUMBO

        MAAFISA AFYA MAZINGIRA DARAJA LA II  WALIO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO
NA      JINA KAMILI     JINSIA  ANUANI  KITUO CHA KAZI
1       WINFRIDA TIBAKYA        F       S.L.P104467 DSM MKURUGENZI WA MANISPAA YA MOSHI

        MAAFISA WATEKENOLOJIA MAABARA   WALIO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO
NA      JINA KAMILI     JINSIA  ANUANI  KITUO CHA KAZI
1       JACKSON E MACHA ME      S L P 317, OLD MOSHI    MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA KOROGWE
2       TEDDY F. MSAKI  KE      S.L.P 480 MOSHI MKURUGENZI WA MANISPAA YA MOSHI
3       JONATHAN J MUFUMYA      ME      S L P 79601, DAR ES SALAAM      MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA MAKAMBAKO


KAIMU KATIBU MKUU

Monday, June 24, 2013

TANZANIA YAPONGEZWA KWA KULINDA HAKI ZA WAKIMBIZI DUNIANI

IMG_7558
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Wakimbizi Dunia ambapo amesema anaishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani katika kuhakikisha Wakimbizi wanakuwa katika mikono salama ya Serikali ya Tanzania.
Kila tarehe 20 ya mwezi Juni Dunia inatambua uwepo wa mamilioni ya Wakimbizi Duniani katika kuhakikisha wanasaidiwa Ili kuondokana na hali ya Ukimbizi katika nchi za ugenini.
Aliendelea kusisitiza kwamba ni vigumu kuelewa Mazingira hatarishi ambayo mkimbizi anayapata kutokana na mapigano ya kisiasa, kidini au kikabila ambayo inawalazimisha kuhama katika makazi yao na kwenda katika makazi ambayo hawayafahamu, alisema watu wasiokuwa na makazi wanazidi kuongezeka Duniani mpaka 2012 takribani watu Milioni 3 walikuwa hawana makazi hizi ni kengele za uamsho wa Jumuiya ya Kimataifa kuamka na kuchukua hatua.
IMG_7577
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Pereira A. Silima akizungumzia majukumu ya Serikali katika kuwahudumia Wakimbizi kutoka nchi za jirani zenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe katika siku ya Wakimbizi Duniani jijini Dar es Salaam.
IMG_7542
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bi. Joyce Mends-Cole akitoa nasaha zake ambapo amesema anatambua uwepo wa Shirika la Wakimbizi nchini Tanzania katika kuendeleza kampeni ya 2011 inayozungumzia umuhimu wa mwamko wa matatizo ya wakimbizi Duniani.
“Sisi Umoja wa Mataifa Tanzia tunasaidia kuhamasisha mwamko huo wa uelewa wa matatizo ya Wakimbizi katika Dunia ya utandawazi ili jamii ijue majanga na madhara ya vita katika familia na kaya”.
Pia ameongeza kuwa Shirika la Wakimbizi Duniani litaendelea kuelimisha madhara ya vita katika nchi zinazoendelea ili kupunguza ongezeko la watu wasiokuwa na Makazi Duniani.
IMG_7569
Balozi wa Marekani nchini Mh. Alfonso Lenhardt na Balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani Mh. Liberata Mulamula wakifuatilia hotuba mbalimbali katika siku ya Wakimbizi Duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa Juma.
IMG_7545
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa maadhimisho hayo.
IMG_7547
Pichani Juu na Chini ni Wageni waalikwa na maafisa mbalimbali wa Umoja wa Mataifa nchini wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakijiri wakati wa maadhimisho hayo.
IMG_7603
IMG_7548
IMG_7546

Ofisi ya CCM Mbinga yachomwa Moto.

  Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi akionyesha sehemu iliyoanzia moto kuwaka na kukamata pazia.
 Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi anayeonekana katika picha akitoa  maelezo kwa nje ambapo walimwaga mafuta aina ya petroli dirishani na kuwasha moto.
 Kama unavyoona katika picha hapo ni ndani ya ofisi baada ya moto kuwaka.
 Huu ni mlango uliomwagiwa mafuta katika upenyo kisha kuwashamoto ambao haukuleta madhara kama walivyo kusudiwa na wachomaji.
Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambao hawapo pichani.
--
Watu wasiojulikana wamechoma moto jengo la ofisi ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma tukio lililotokea Juni 21 mwaka huu majira ya usiku pamoja mlinzi wa ofisi hizo kuwepo katika eneo hilo la ofisi mpaka majira ya saa 12 asubhi  na hakuweza kutambua kutokea kwa kitendo hicho kilichofanywa na watu wasiojulikana usiku huo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi amesema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni 21 mwaka huu ambapo watu wasiojulikana walichoma moto moja ya jengo la ofisi za chama hicho wilayani humo  moto ambao ulielekelezwa katika chumba cha ofisi ya katibu ambapo walivunja vioo na kuchoma moto mapazia lakini kabla hawajachoma vitu vilivyokuwemo ndani walikimbia na kuacha dumu lililokutwa likiwa na mafuta aina ya petroli.

Alisema kuwa mpaka sasa hakuna hisia zozote zinazohusiana na tukio hilo ingawa uongozi wa chama cha mapinduzi wilayani humo umeshatoa taarifa kwenye vyombo ya ulinzi na usalama ambavyo vinaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Katika hatua nyingine hali ya sintofahamu imejitokeza katika uchaguzi wa viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga baada ya halmashauri hiyo kugawanywa na kuzaliwa kwa halmashauri mpya ya wilaya Nyasa kwa kuibuka kwa vitendo vya hujuma vinavyodaiwa kufanywa dhidi ya  mgombea mmoja wa nafasi ya mwenyekiti jina lake kuenguliwa katika mazingira ya kutatanisha na kuzua maswali mengi miongoni mwa madiwani wa halmashauri pamoja na wananchi na kutaka uchaguzi huo usifanyike mpaka majina yote matatu ya wagombea yawepo.

Mmoja wa wananchi wa halmashauri hiyo ya wilaya ya Mbinga ambaye pia ni katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi  wa kata ya Mbinga mjini Monika John alisema kuwa hizo ni dalili za kuwepo kwa njama za wazi za kupanga safu ya uongozi ambao siyo chaguo la walio wengi bali ni chaguo la baadhi ya viongozi wa halmashauri hiyo kwa masilahi yao.

Akizungumzia hali hiyo katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mbinga alisema kuwa uteuzi wa wagombea wa nafasi hizo hufanywa kwa kuzingatia kanuni za chama na wenye jukumu la mwisho  la uteuzi ni uongozi wa chama ngazi ya mkoa  na yeye si msemaji wa maamuzi ya ngazi mkoa ingawa amepokea tarifa ya kusitishwa kwa uchaguzi huo mpaka taarifa nyingine itakapotolewa na ofisi ya chama ngazi ya mkoa.

Picha na Habari kwa hisani ya demashonews

PICHA ZA WAZIRI MKUU MHE. PINDA AKIFUNGUA MKUTANO WA MADC, MARC NA MARAS BUNGENI MJINI DODOMA

Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakinukuu maelekezo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua  Mafunzo  ya Kujenga Uwezo kwa Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Mikoa kwenye ukumbi wa Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma  Juni 24,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu IMG_0037 
Baadhi ya Wakuu wa  Wilaya wakimsikiliza  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua  Mafunzo  ya Kujenga Uwezo kwa Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Mikoa kwenye ukumbi wa Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma  Juni 24,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu MizengoPinda akihutubia wakati alipofungua  Mafunzo  ya Kujenga Uwezo kwa Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Mikoa kwenye ukumbi wa Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma  Juni 24,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0055 
Waziri Mkuu MizengoPinda akihutubia wakati alipofungua  Mafunzo  ya Kujenga Uwezo kwa Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Mikoa kwenye ukumbi wa Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma  Juni 24,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0118 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa mkuranga na  Waziri wa Kilimo na Ushirika, Adam Malima, Bungeni mjini Dodoa Juni 24, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0143 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na wabunge, Bungeni Mjini Dodoma 24,2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0149 
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiteta na Wabunge Mary Chatanda wa Viti Maalum (kushoo)  na  Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi Hillaly kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 24, 2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0150 
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiteta na Wabunge Mary Chatanda wa Viti Maalum (kushoo)  na  Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi Hillaly kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 24, 2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0161 
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (kushoto) na Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi  Hillaly kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 24, 2013. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (kushoto)  kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 24, 2013. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)IMG_0177 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi  Hillaly kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 24, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KUHUSU UPOTOSHAJI WA JOYCE KIRIA

Advera-SensoInasikitisha kuona kwamba huyu mama Joyce Kiria anaingilia mambo ya kisheria na kutaka kupotosha jamii kwamba hajui mume wake yuko wapi pia nadhani analenga kuichochea jamii kwamba aliyetuhumiwa kutenda uhalifu akikamatwa familia yake iandamane, tendo ambalo pia ni kosa la jinai. Aidha anatakiwa kuheshimu haki za watoto na kuacha kuwatumia katika kinga ya kutetea watu wanaotenda uhalifu (Imetolewa na Advera Senso Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini Tanzania)
1a 
Joyce Kiria akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam ambapo alidai hajui mume wake yuko wapi

From The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation

 Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation this morning received copies of Credentials from the Designate Ambassador T. Raveenthiran of Sri Lanka to the United Republic of Tanzania with offices in Nairobi, Kenya.
 Hon. Membe in a discussion with Designate Ambassador Raveenthiran (center) of Sri Lanka and a Senior Officer in the Sri Lanka Embassy during their meeting in Dar es Salaam this morning. 
Hon. Minister Membe explains something during his discussion with Designate Ambassador Raveenthiran of Sri Lanka in his office in Dar es Salaam.
 Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation receiving copies of Credentials from Designate Ambassador Ittiporn Boonpracong of Thailand to the United Republic of Tanzania with offices in Nairobi, Kenya.
 Hon. Bernard K. Membe in a discussion with Designate Ambassador Ittiporn Boonpracong of Thailand.  Also in the photo is Mr. Omary Mjenga, Assistant Director of the Department of Asia and Australasia in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation and Ms. Sudkanueng Nivestratana, Second Secretary in the Royal Thai Embassy.
Hon. Bernard K. Membe (MP), explaining something during his discussion with Designate Ambassador Ittiporn Boonpracong of Thailand during their meeting this morning in Dar es Salaam.
 Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation receives copies of Credence from Designate Ambassador Shesudin Ahmed Roble of Ethiopia to the United Republic of Tanzania with offices in Nairobi, Kenya.  The ceremony took place earlier today in the Minister's office in Dar es Salaam.
 Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation thanks Designate Ambassador Roble of Ethiopia at the end of their meeting earlier today in Dar es Salaam.
 Hon. Bernard K. Membe (MP) (right), listening carefully to Designate Ambassador Shesudin Ahmed Roble during their meeting earlier today.
Hon. Minister Membe in a candid moment with Designate Ambassador Roble of Ethiopia and his Embassy Counsellor Eskindir Y. Asfaw. All photos by Tagie Daisy Mwakawago-Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation

JESHI LA POLISI MKOANI RUVUMA LAKAMATA MENO 18 YA TEMBO.

Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma  Deusdedit Nsimeki akipanga maneno ya tembo kulingana na uneno /uzito kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
 Mwandishi wa habari wa katika Gazeti la Mtanzania Hamoni Mtega akiwa amenyanyua jino la tembo
-------------------------------------------------- 

JESHI  la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kukamata meno ya Tembo  18 yenye uzito wa kilo 84 yenye  thamani ya Tsh216,000,000/ambapo meno hayo 18 ni sawa na dola 15 elfu za kimarekani pia ni sawa na Tembo tisa waliouwawa .
 
 Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo Kamanda wa polisi mkoani Ruvuma  Deusdedit Nsimeki amesema kuwa tukio hilo la kukamata meno hayo lilitokea Juni 20 Mwaka huu majira ya saa 3.00 usiku  katika kijiji cha Majala kata ya Nandembo iliyopo wilaya  ya Tunduru mkoani Ruvuma .
  
 Kamanda Nsimeki amesema kuwa  tukio hilo la kukamatwa kwa meno hayo ya tembo lilitokea  baada ya askari polisi wa wilaya hiyo kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ndipo wao waliweka mtego wa kuwanasa watuhumiwa hao lakini bahati mbaya watuhumiwa hao walikurupuka na kuacha mizigo ya meno hayo iliyokuwa imefungwa kwenye mifuko tofauti tofauti.
   
 Alisema kuwa watuhumiwa waliokurupuka walikuwa wanne huku kila mmoja na baiskeli ambazo walikuwa wamebebea meno hayo na kwa upande wa watuhumiwa wa meno ya tembo kukurupuka bila kutiwa mbaroni na jeshi hilo limekuwa ni tukio la pili la kwanza  lilitokea katika  kijiji  cha Hanga wilayani Namtumbo na la pili ndiyo hilo la wilaya ya Tunduru zote za mkoani Ruvuma .
  
 Aidha kamanda alisema kuwa jeshi la polisi linajitahidi kuwasaka watu ambao wamejificha na wanajihusha na matukio hayo ya ujangili kwa wanyama  na hasa tembo.
             
Pia ametoa wito kwa wananchi uendelea kushirikiana jeshi la polisi mkoani Ruvuma kwa kutoa taarifa za siri zitakazowezesha kukamatwa kwa wahusika wa vitendo vya uhalifu wa aina yoyote kwa sababu suala la ulinzi ni kila mmoja hivyo kunasoaswa kuwepo kwa ushirikiano wa karibu baina ya polisi na wananchi.
 
VIA/demashonews

Monday, June 17, 2013

WAJUMBE WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA MKOA WA RUVUMA WAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YA MANISPAA YA SONGEA

 Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakikagua mradi wa  vyanzo vya Maji vilivyopo katika mlima  Matogoro mjini Songea,
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakikagua mradi wa Kibanio cha umwagiliaji katika kata ya Subila iliyopo Manispaa ya Songea
Banio hili limegharimu kiasi  cha Tshs Milioni Mia mbili ishirini hadi kufikia hapa lilipo.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi kinachojengwa katika eneo la Msamala kwa mfumo wa JENGA ,ENDESHA,KABIDHI.
Mfumo huu unamuwezesha mwananchi kujenga kibanda nakukitumia kwa mkataba wa miaka kumi na moja kisha anakabidhi halmashauri ya Manispaa ya Songea.Hata hivyo wajumbe walihoji juu ya ujenzi huo na ukubwa wa eneo kulingana na ongezeko la watu, magari na huduma nyinginezo katika eneo hilo kuwa haliwezi kukidhi ongezeko hilo kutokana na eneo hilo kuonekana dogo.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiendelea kuhoji juu ya ujenzi wa kituo hicho kipya  cha Mabasi ambacho kimezua utata miongoni mwa wajumbe hao.
Toka kushoto ni katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamedi Maje akiwa na mjumbe kutoka wilayani Tunduru wakiwa wameshikwa na butwaa baada ya taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa kituo hicho cha Mabasi
Kaimu Mhandisi wa Manispaa ya Songea Davis Mbawala  akijibu maswali ya wajumbe juu ya ujenzi wa kituo kipya cha mabasi kinachojengwa kwa mfumo wa JENGA,ENDESHA,KABIDHI,
Toka kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga, Mwandishi wa habari wa ALAT mkoa wa Ruvuma Nathan Mtega na mkurugenzi wa Halmashauri ya Namtumbo ambaye pia ni Katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamed Maje wakiwa katika picha ya pamoja
Katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamed Maje akiteta jambo na Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga wakati wa majumuisho ya ziara ya wajumbe wa ALAT baada ya ukaguzi wa miradi
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiwa ndani ya ukumbi wa mkutano
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru akitoa hoja katika kikao cha majumuisho baada ya ziara ya kukagua miradi
Mwandishi wa habari Cresencia Kapinga akitoa mapendekezo katika kikao cha majumuisho.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Tunduru Robert Nehata akiuliza swali
katibu ALAT Mohamed Maje akizungumza kabla ya kumkaribisha mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho