Tuesday, January 21, 2014

Hongeraaaaa Mpiganaji Juma Nkamia


Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Juma Selemani Nkamia akipokewa na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Clement Mshana, katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Olegabriel

Hongera saaaaana Juma Nkamia.

Najua kwa pongezi hizi wapo ninaowaudhi lakini naomba wadau tujenge utamaduni wa kukubali mafanikio ya binadamu. 

Nampongeza Juma Seleman Nkamia, mwanahabari wa siku nyingi na mbaye pengine amekua kichocheo cha wana habari wengi wanaofanya vizuri hii leo kutokana na umahiri wake wa utangazaji.

Juma umetutoa kimasomaso, umetupa heshima unatuwakilisha. Sina mengi zaidi na sitaki kuzua mjadala naomba niikamilishe furaha yangu kwa kusema Cheza karata yako vizuri utusafishie njia sote tuliofurahi na wasiofurahi. Ukweli ni kwamba wewe ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Kwani kitu gani eheee, Kaji moja bana. Ahahahahaaaaa!!!!!