Wednesday, August 7, 2013

Sunday, August 4, 2013

Taja Mmoja mmoja

Kutoka shoto............... 
 Wapiganajiiiiiiiiiiii
Da' Kele akipiga boksi, utaumiaaaa!!!! Ohooooo!!!!! 
Ka' Mtega na nanii hii wangu.

Wapiganaji wakipiga boksi

Mwenye nani hii twende, mwenye kanani hii twende. Hata Mchina ruksa ahahahaaaaa

Chindiye na Mrs nani hiii


wako?????

Rais Mstaafu Clinton Amtembelea Dr Shein Ikulu zenji


RAIS MSTAAFU WA MAREKANI BIN CLINTON.NA RAIS DK.SHEIN


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake.

Saturday, August 3, 2013

Wadau mnamkumbuka Mwandishi wa Habari Mkongwe Agustino Mbunda?


Huyu ndiye Agustino Mbunda.

Leo nje ya mkutano wa kawaida waandishi wa habari katika Mkoa wa Ruvuma, nimekutana na Mwandishi wa habari wa Siku nyingi Mzee Agustino Mbunda.

Nimefurahi kukutana nae kwa sababu ni miongoni wapiganaji waliofanya kazi kubwa ya kuwaelewesha watanzania juu ya umuhimu wa fani hii.

Kwa wenye kumbukumbu Agustino Mbunda ndiye aliyefichua kashfa ya meno ya tembo mwaka 1988 iliyomhusisha aliyekua mbunge wa Songea Mjini Abdulabi Ally Yusuf, ambaye alitiwa hatiani na mahakama kuu na kuhukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 12 Jela.

Mbunda pia ndiye aliyeandika habari kuhusu ugonjwa wa mihogo uitwao Cassava Mealbug ambao uliathiri mashamba mengi na kutishia Hali ya chakula. Maeneo yaliyoathirika ni pamoja ukanda wa mwambao wa ziwa Nyasa. Habari hii ndio ililazimu serikali kuagiza manyigu kutoka nchini Nigeria kwa ajili ya kukabiliana na wadudu wa cassava Mealbug. Inasemekana tatizo lilikomeshwa kutokana na kupandikizwa kwa manyigu hayo ambayo yapo hadi Leo.

Mkongwe huyu wa Habari pia aliandika historia miaka ya mwanzoni mwa 1980, (Tarehe kamili nasearch) aliporipoti juu ya mchezo mchafu unaofanywa na menejimenti ya ghala la mbolea la Makambako Mkoani Iringa, ambapo wakulima walikua wakinyanyaswa kupewa mbolea kwa kuwekewa ukiritimba huku mbolea hiyo ikipelekwa kwa wafanyabiashara na kuuzwa kwa bei juu. Aliyekua waziri Mkuu wakati huo Edward Moringe Sokoine alisafiri usiku kucha hadi Makambako na akafika na kukuta meneja wa ghala hilo kalala, akatuma mtu akamwamshe na alipofika na kuulizwa akakosa majibu na hapohapo kikaota nyasi

Pia aliandika habari kuhusu simba wala watu Tunduru, kukatokea upinzani kutoka kwa baadhi ya maafisa wanyamapori. Mmojawao akaamua kwenda Tunduru na yaliyomkuta nae akaliwa na Simba.

Big Up Mzee Mbunda, tupo pamoja and we are proud of you Sir


























Ruvuma Press wafanya mkutano wao wa kawaida, Mwambungu atoa neno.



Chama cha waandishi wa habari Mkoani Ruvuma Leo kinaendesha mkutano wake wa kawaida. Mgeni rasmi ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ambaye pamoja na mambo mengine amesisitiza umuhimu wa waandishi wa habari kuwa makini katika kazi zao kwa kuhakikisha wanaanza kazi yenye kuwasaidia watanzania kukabiliana na changamoto za maisha ikiwemo kupambana na umasikini.

Aidha Mwambungu ameonya kuwa waandishi wa habari waepuke kuwa mawakala wa kuzalisha milipuko inayovuruga amani na kuleta mifarakano katika jamii.

Mkuu Huyu wa Mkoa ambaye amekua kipenzi wa karibu wa vyombo vya habari pia ametaka waandishi wa habari wajenge tabia ya kupendana, waache kuchimbanachimbana na Daima wajadili mambo yenye manufaa kwao na wananchi wanaowahudumia.

Katika Mkutano huo Katibu wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoani Ruvuma Andrew Chatwanga amemuomba Mkuu wa Mkoa na Meya wa Manispaa hiyo Charles Mhagama wasivunje jengo la kitega uchumi la chama hicho lililopo katikati ya mji ambalo Manispaa iliidhinisha livunjwe kutokana na taratibu za mipango miji.

Mwambungu amekubali ombi Hilo na ameisihi Manispaa ya Songea iongeze mwaka mmoja kwa Jengo Hilo kuendelea kuwepo.

Chatwanga pia amemuomba Mkuu wa Mkoa Mwambungu akisaidie chama hicho kutunisha mfuko kwa ajili ya mradi wa uanzishaji wa kituo cha Radio ambacho ununuzi wa vifaa na studio unaendelea kwa kutegemea michango ya wadau.