Thursday, March 6, 2014

Msaada wadau kutambua majina ya wachezaji hawa wa Majimaji FC enzi hizo za Dr Gama

 

Mdau Mpenda Mvula Kanijaalia picha hii ya timu ya Majimaji ya Songea Enzi hizo za Bambo Gama (Dr Laurence Gama) lakini kanipa mtihani kutafuta majina ya kila mchezaji hapo. Msaada wadau.
 
Huyu ni Mzee Abdalah Ally, Mmoja wa waasisi wa timu ya Majimaji. Yeye na wenzake akina Mbegambega walikua na timu zao za soka zilizokua na nguvu Songea, alipokuja Dr Gama akawashawishi wavunje timu zao na kuunda timu ya Majimaji na wao wakawa viongozi. Kuna
habari kuwa Mzee huyu alikua mpenzi Mkubwa wa Majimaji FC kiasi kwamba miaka ya 80 Majimaji ilipofungwa na Yanga alipatwa na Upofu, Namtafuta mwanae Hamis Abdalah Ally athibitishe habari hizi. Mzee huyu ametangulia mbele za Haki Machi 02, 2014
siku ambayo Majimaji ilicheza dhidi ya Lipuli ya Iringa na Lipuli ilichapwa 2-0.