Saturday, August 31, 2013
Friday, August 30, 2013
Breaking news!!!! Marekani yatangaza kuwa Serikali ya Bashar al-Assad imeua watu 1429 kwa silaha za sumu nchini Syria
John Kerry - Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani,
Alipokua akitoa taarifa kwa vyombo vya habari katika Ikulu ya Marekani (White House)
Na Msigwablog
Muda mfupi uliopita Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry amezungumza na vyombo vya habari na kutangaza rasmi kuwa serikali ya Marekani inajua na ina uhakika wa ushahidi kuwa serikali ya Syria ya Rais Bashar al-Assad imehusika kuwaua watu 1429 wiki iliyopita kwa kutumia silaha za sumu. Kerry amebainisha pia kuwa Kati ya watu Hao wamo watoto 426 waliouawa kwa silaha hizo za sumu.
Aidha Kerry anasema serikali ya Syria imekua ikitumia silaha za sumu na hiyo ni sehemu ya mkakati wake wa kukabiliana na maadui wake huko mashariki ya Kati.
Aidha Waziri Huyu wa mambo ya nje wa Marekani anasema Rais Obama Anajua kuwa kukabiliana na tatizo la Syria kutakua na madhara makubwa lakini potelea mbali.
Haya sasa wadau, shughuli nyingine pevu inanukia Syria.
Rais wa Syria Bashar al-Assad
Mtuhumiwa wa kutumia silaha za sumu wiki iliyopita kulikosababisha vifo vya watu 1429
Mwaka huu Mahindi ya Chakula bweleleeeee!!!!
Haya ni mahindi yanayonunuliwa na NFRA katika kituo chao cha Mbozi Mkoani Mbeya
Na; Msigwablog
Msimu huu wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA, wamefanikiwa kukusanya zaidi ya tani 160,000 za mahindi kati ya tani zote 200,000 wanazokusudia kununua kutoka kwa wakulima. Mkoani Ruvuma peke yake tayari wamenunua tani 36,000 kati ya tani zote 50,000 wanazotarajia kununua msimu huu
Hali hii imevunja rekodi kwa kuwa Mahindi yamenunuliwa kwa kasi kubwa. Matharani mwaka jana, mahindi kama haya ya safari hii yalinunuliwa kwa muda wa miezi sita lakini safari hii ni ndani ya mwezi mmoja.
Mkurugenzi Mkuu wa NFRA Charles Warwa anasema pamoja na wao kununua mahindi hayo, pia wanaendelea kuzijizatiti kwa kujenga maghala mengi zaidi ili waweze kuhifadhi mahindi yote ndani ya maghala badala ya kuyahifadhi nje.
Mwaka huu NFRA imefanikiwa kupata mahindi mengi kutokana na kununua mahindi kwa bei nzuri ya shilingi 500 kwa kilo moja inayomfikia mkulima moja kwa moja, hali ambayo kwa Mkoani Ruvuma wanunuzi wengine binafsi wameshindwa kuifikia bei hiyo na hata mahindi yao nao wanayapeleka kwa NFRA
SWALI NI JE????
Baada ya NFRA kumaliza kununua tani zao 200,000 kwa msimu huu, wanunuzi binafsi wataendelea kununua mahindi ya wakulima kwa shilingi 500 kwa kilo moja? au ndio mwanzo wa Majanga?
Tuesday, August 27, 2013
Hili linaudhi wadauuuuuu!!!
Ndugu zangu???????
Hakuna jambo linanikera wakati wa kazi unakuta mpiganaji anakuja kwenye interview na simu ya Mkononi tena mchina kwa ajili ya kurekodi sauti, halafu anaisogeza mdomoni mwa anayehojiwa.
Kwa wapiga picha this is very unfair. Jamani nunue voice recorder na bei zake sio ghali kivile. tuweke microphone tuonekane serious people.
Na ujumbe huu uwafikie Wamiliki wa vyombo vya habari, wanunulieni waandishi wenu wa habari Voice Recorder, msitake vipindi vya chee kama ni live transmission basi nunue teleporters
Lets change guys!!!!
Monday, August 19, 2013
Nakumbuka Kama vile kulikua na Kampeni ya kuondoa utitiri wa Minara ya simu, radio, TV nk?
Haya kila anayetaka kurusha matangazo ajenge Mnara wake na vijumba vya walinzi na mafundi.
Aweke uzio na majenerator yake ya kufua umeme.
Na pia aweke solar power system yake.
Minara hiyo yoooote ingeweza kuwa mnara mmoja na kila mmoja akakobeka virusha matangazo yake hapo. Tafakari..........Chukua hatua.
Wangapi wanamuunga Mkono Dr Harrison Mwakyembe????????
Nimebahatika kutazama live kipindi cha Jenerali On Monday Chanel Ten. Dr Mwakyembe akizungumza na David Ramadhan kuhusu Shughuli aliyoianza ya kukomesha upitishaji wa dawa za Kulevya viwanja vya ndege na bandari
Akisisitiza "Hakatizi mtu na dawa za kulevya bila kubambwa"
Uwanja wa Ndege wa Dar es salaam, wenye kashfa ya kutumiwa kupitisha dawa za kulevya
Subscribe to:
Posts (Atom)