Friday, August 9, 2013

Billionare Oprah Winfrey aonja joto ya ubaguzi wa rangi Uswisi

Oprah Winfrey 

Habari kutoka nchini Uswisi zinasema tajiri mwanamke dunia Oprah Winfrey Raia wa Marekani mwenye asili ya Africa ameonja joto ya jiwe alipoingi katika duka moja nchini Uswisi, pale muuza duka alipokataa kumpa mkoba wa kike (Kipima joto) wenye thamani ya Pauni 24,477 sawa na shilingi milioni 61 kwa madai kuwa hana uwezo wa kumudu gharama za kuununua mkoba huo.

Oprah amekitafsiri kitendo hicho kuwa ni ubaguzi wa rangi, akiamini kuwa muuza duka huyo alimuona kuwa kwake mtu mweusi hawezi kuwa na uwezo wa kununua mkoba huo.

Oprah Winfrey anayetajwa kuwa moja ya matajiri wakubwa wanawake dunia mwenye asili ya Africa anadai alikwenda dukani hapo akiwa simple, na hakukua na viashiria vya mtu maarufu ambaye kwa kawaida hutembea na watu wengi kwa ajili usalama na huduma nyingine anasema alipoingia dukani hapo alipendezwa na mkoba huo uliokua umewekwa ukutani na ndipo alipotaka kuuona ili afanye uamuzi  wakuununua ama la.

Alikwenda nchini Uswisi kuhudhuria harusi ya Tina Turner.

Anasema aliomba mara ya kwanza, muuzaji akamwambia mkoba huo ni ghrama mno hawezi kuimudu bei yake, akauliza mara ya pili bado akapewa jibu hilo hilo na akauliza mara ya tatu bado akapewa jibu hilo hilo hadi alipoamua kuondoka dukani hapo.

mmliki wa duka hilo Trudie Goetz ameomba radhi kwa lililotokea.

Hata hivyo Oprah amekiri kuwa pengine alijibiwa hivyo kwa kuwa muuzaji hamfahamu na kwa sababu Vipindi vyake "Oprah shows" si maarufu nchini Uswisi.

Tayari Oprah Winfrey ametunukiwa tuzo ya ya Rais ya heshima ya juu ya Uraia nchini Marekani ambayo atakabidhiwa na Rais Barack Obama katika Ikulu ya Marekani (White House) Baadaye Mwaka huu.

Haya wadau habari ndio hiyo, Dada ana mihela ya kumwaga hadi anashangazwa na muuza duka anayeona so kumuuzia mwafrika mkoba wa milioni 61.