Saturday, July 20, 2013

Taswira:Ziara ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda mjini Mbinga, Pia Ashuhudia Upakuaji wa Mabomba ya Gesi Bandari ya Mtwara

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akialimiana na Leah Kayombo, Mke wa Mbunge wa Mbinga Mashariki, Gaudence Kayombo baada ya kuwasili mjini Mbinga akitoka Nyasa kwa ziara ya mkoa wa Ruvuma, July 18, 2013.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Madaktari  wa kujitolea Kutoka Korea ya Kusini na Laos wanaofanya  kazi  katika hospitali ya wilaya Mbinga , Julai 18, 2013. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma. 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kuzindua utelemshaji wa mabomba ya gesi kutoka kwenye meli kwenye bandari ya Mtwara Julai 18, 2013. Mabomba hayo yatatandikwa chini ya ardhi kusafisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es salaam.  Kulia kwake ni Balozi wa China nchini, Dr. Lu na Kulia ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini , Stephen Masela. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia. 

Wairi Mkuu, Mizengo Pinda akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia (wapili kushoto) wakati alipozindua utelemshaji wa mabomba ya gesi kutoka kwenye meli kwenye bandari ya Mtwara, Julai 18, 2013. Mabomba hayo yatatandikwa ardhini ili kuwezesha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara hadi Dar es salaam. 
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na  Hassan Kasuguru,nahodha alieingiza bandarini  Mtwara meli yenye mabomba ya gesi kutoka China wakati alipozindua upakuaji wa mabomba hayo  Julai 18, 2013.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Balozi wa China nchini, Dr. Lu kabla ya kushuhudia upakuaji wa mabomba ya gesi kwenye bandari ya Mtwara , Julai 18, 2013. Mabomba hayo yatatandikwa ardhini ili kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es salaam.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu