Sunday, July 7, 2013

Uchunguzi Ajali ya Ndege ya San Francisco unaendelea



Taswira za ajali ya ndege na uchunguzi unaoendelea
 Moto Mkubwa ulifuka kabla ya vikosi vya zimamoto havijaudhibiti   


Hatimaye imefahamika kuwa idadi ya waliosalimika katika ajali ya Ndege iliyotokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa San Francisco Nchini Marekani ni 305 na ni watu wawili ndio waliopoteza maisha. Kati ya waliosalimika wati 182 walilazwa Hospitali na wengine 123 walitibiwa na kurejea  kuondoka. 

Uchunguzi zaidi kuhusiana na ajali hii bado unaendelea kufanyika. Ndege hii inaendeshwa na kampuni kubwa kuliko zote huko Korea Kusini iitwayo Asiana Airlines. Ndege yenyewe ni aina ya Boeing 777 na ilikua ni ndege namba 214. 

Imethibitika kuwa Ndege hii ya injini mbili ilikua na abiria 291 na wafanyakazi 16 na iliruka kutoka uwanja wa Ndege wa Seoul  Korea Kusini na kusafiri kwa takribani saa 10 kabla ya kukutwa na ajali wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa San Francisco

Waliofariki dunia ni Binti Ye Mengyuan na Wang Linjia wote ni raia wa China na walikaa katika viti vya nyuma ya nege ambapo ndiko mshindo mkubwa wa kuanguka ulikopiga.