Thursday, May 23, 2013

Tahariri ya Gerson Msigwa inakuja kaa tayariiiiiii


Tahariri ya Gerson Msigwa.
Awali ya yote napenda kuwapongeza na kuwashukuru wasomaji wote Blog yangu.
Nawaahidi kuwa pamoja na majukumu yanayonikabili katika ujenzi wa Taifa, hamtajutia kunitembelea katika Blog hii na ukurasa wangu wa Facebook.
Nimeamua kwa dhati kuwa na ukurasa wa “Tahariri ya Gerson Msigwa” Mahali hapa nitakua nikimulika kitaaluma, kwa uchambuzi mfupi juu ya yale ninayoyaamini katika fani hii ya uandishi wa habari. Kwa maoni yangu hapa ndipo mahali ninapoweza kutoa mchango wangu wa mawazo kuhusu fani hii na mimi naamini kuwa itakua mahali muafaka pa kukirithisha kizazi kinachonifuata juu ya fani hii ya uandishi wa habari. Sina maana kuwa kila nitakachoandika hapa ni msahafu, hapana. Ni maoni yangu tu.
Hivyo basi nawaalika wadau kushirikiana name katika safu hii, na nyie pia mnaweza kutoa maoni yenu ili mradi tujadili mambo kwa faida ya fani ya uandishi wa habari tuliyoisomea na tunayoitumikia.
Tahadhari; Tahariri zangu zote hazitakua na mtazamo wowote wa Kisiasa, Kidini, Kikabila wala Kikanda na naomba hata mtakaopendezwa kushiriki mjadala muongozwe na mtazamo huo. Kwa niliowakwaza kwenye hili wanisamehe kwa sababu mimi ni miongoni mwa watu wanaoamini kuwa binadamu wote ni sawa, dini, siasa, kanda na makabila havina faida yoyote kuvishabikia.
Yatakayokuwemo kwenye tahariri hii ni yangu binafsi na hayahusiani na taasisi yoyote wala mamlaka yoyote, wala kikundi chochote, wala tabaka lolote nakadharika.
Kwa hiyo, Karibuni wadau.