Wednesday, May 8, 2013

Viongozi wa dini wapata mafunzo ya mapambano dhidi ya rushwa



MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU WA PILI KUSHOTO AKIWA PAMOJA NA MKURUGENZI WA MKUU WA TAKUKURU DKT EDWARD HOSEA NA KATIKATI NA KAMANDA WA TAKUKURU MKOA WA RUVUMA DAUD MASIKO  KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WATUMISHI WA TAASISI HIYO MKOANI RUVUMA

........................................

Chanzo;Demashonews

 IMEELEZWA kuwa mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa nchini ambavyo vinazidi kuongezeka siku hadi siku ni jukumu la kila mmoja katika jamii ikiwa ni pamoja na viongozi wa serikali na viongozi wa  taasisi za kidini kwa sababu rushwa ipo katika mihimili yote ya serikali huku baadhi ya vitendo vya viongozi na mfumo wa uongozi ukiruhusu kuwepo kwa mianya ya rushwa.

 

 Akizungumza katika mafunzo ya siku moja kwa viongozi wa madhehebu ya dini ya kiislamu na kikikristo wa mikoa ya Iringa,Njombe na Ruvuma yaliyofanyika mjini Songea mkoani Ruvuma Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Dkt Edward Hosea alisema kuwa kutokuwepo kwa uwazi,uwezo wa uwajibikaji wa viongozi na watendaji wa serikakali kuwepo kwa mianya ya rushwa.

 

 Alisema kuwa kwa sababu maadili ya umma yametiwa unajisi mbele ya madhabahu ya kidini na hasa nyakati za chaguzi mbali mbali taasisi imeona umuhimu wa kuwashirikisha viongozi wa dini mbili kubwa hapa nchini kwa kuwapatia mafunzo ya namna ya kudhibiti na kupambana na rushwa kwa sababu rushwa ni suala mtambuka linalogusa kila eneo na kila mwananchi.

 

 Dkt. Hosea aliwaambia viongozi hao wa dini kuwa kutoa na kupokea rushwa ni dhambi lakini pia ni kosa la jinai hivyo kuna kila sababu ya kutafakari kwa pamoja namna ya kuitokemeza rushwa kwa umnoja wa taifa  na siyo busara kuliacha jukumu hilo mikononi mwa taasisi hiyo pekee kwa sababu wahusika wa rushwa wapo katika kila sekta na hasa sekta zinaziotoa huduma kwa wananchi.

 

 Akizungumzia mianya ya kukuwa kuwa vitendo rushwa nchini ni pamoja na kuwepo kwa mapungufu katika utawala bora na uwajibikaji wa viongozi na watendaji wa sekali na sekta binafsi ikiwa ni pamoja na ukiukwaji wa utawala wa kisheria kwa baadhi ya viongozi na watendaji wa sekta zinazotoa huduma kwa umma kwa kutokuwepo kwa uwazi na uwezo thabiti wa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

 

 Akizungumzia madhara ya rushwa kwa jamii alisema kuwa mtu mwenye kipato cha chini ndiye muathirika mkubwa wa rushwa kuliko mwenye kipato kikubwa kwa sababu mwenye kipato cha chinji hulazimika kutoa rushwa kubwa huku mwenye kipato kikubwa akitoa rushwa ndogo na vitendo hivyo huambatana udanganyifu,wizi,ubadhirifu na mmomnyoko wa maadili na viwango vya rushwa kwa kwa watu wenye kipato cha chini kikiwa ni asilimia 3.3 huku wenye kipato kikubwa ni asilimia 0.9.

 

  Akijibu maswali ya baadhi ya viongozi wa dini waliotaka kufahamu juu ya utendaji wa taasisi hiyo katika kushughulikia rushwa kubwa ambazo zimekuwa zikilalamikiwa nia wananchi walio wengi alisema taasisi imepewa mamlaka ya kuchunguza lakini mamlaka ya kushitaki ya kwenye ofisi ya mwendesha mashitaka wa serikali kwa mfumo wa muundo  wa taasisi hiyo ya kuzuia na kupambana na rushwa hauipi tasisi iwezo wa kushitaki bal;I kuchunguza.

 

Awali akifungua mafunzo hayo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu  mbali ya kumpongeza mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini kwa uamuzi wa kuendesha mafunzo kwa viongozi dini kuhusu mapambano dhidi ya rushwa lakini aliwaomba viongozi wa dini kusaidia katika jukumu la kudumisha amani na utulivu wa nchi kama ulivyoasisiwa na waasisi wa taifa.