Thursday, May 16, 2013

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA RELI, BARABARA, VIWANJA VYA NDEGE


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahaman Kinana akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa wawekezaji wa sekta binafsi (CEO Round Table Dinner) uliofanyika juzi usiku katika hoteli ya Kilimanjaro Kempiski.


Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahaman Kinana amesema ubinafsishaji haujafanikiwa vizuri kwani tangu sera hiyo ianze nchini kuna viwanda havifanyi kazi wala kutoa ajira kama ilivyokusudiwa na hivyo serikali ya Chama cha Mapinduzi inahitaji wawekezaji wa sekta binafsi katika kuboresha huduma katika reli, barabara na viwanja vya ndege.


Akizungumza jana na waandishi wa habari, pamoja na wawekezaji wa sekta binafsi katika mkutano ulifanyika juzi usiku katika hoteli ya Kilimanjaro Kempiski.

Sera ya CCM ipo wazi, tunawahitaji wawekezaji wa sekta binafsi na tumekuwa tukiwahitaji tangu siku zote, lazima kwanza tutambue uwepo wao ili tuweze kuwashirikisha katika sekta ya kusaidia jamii katika hhudma za jamii

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi amezungumza na wawekezaji wa sekta binafsi, mwezi mmoja tangu katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) naye kuzungumza na wawekezaji hao. Wakurugenzi hao hukutana na vyama mbalimbali kujua sera zao vyama na ushirikiano wao na sekta binafsi nchini.
 
Credits: Habarimseto blog