Monday, June 3, 2013

Yambesi ataka wananchi vijijini wakumbukwe kwa TEHAMA


Katibu Mkuu ofisi ya Rais na utumishi wa umma Bw George Yambesi akijadiliana jambo na Rais wa (AADCL) na Mkurugenzi (DLC) kutoka  Senegal Bwana Mor Seck, kushoto kwa Yambesi ni Mkurugenzi mtedaji wa (TAGLA) Charles Senkoro.



Katibu mkuu wa ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma GEORGE YAMBESI amewataka wajumbe wa umoja wa vituo vya elimu kwa njia ya mtandao barani AFRIKA washirikiane na makampuni ya TEHAMA na simu za mikononi kuwafikishia elimu wananchi walio maeneo ya Vijijini. Bwana Yambesi ndiye aliyeufungua mkutano huo leo.

Picha na Mpiganaji Mahili Chris Mfinanga