Monday, June 17, 2013

WAJUMBE WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA MKOA WA RUVUMA WAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YA MANISPAA YA SONGEA

 Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakikagua mradi wa  vyanzo vya Maji vilivyopo katika mlima  Matogoro mjini Songea,
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakikagua mradi wa Kibanio cha umwagiliaji katika kata ya Subila iliyopo Manispaa ya Songea
Banio hili limegharimu kiasi  cha Tshs Milioni Mia mbili ishirini hadi kufikia hapa lilipo.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi kinachojengwa katika eneo la Msamala kwa mfumo wa JENGA ,ENDESHA,KABIDHI.
Mfumo huu unamuwezesha mwananchi kujenga kibanda nakukitumia kwa mkataba wa miaka kumi na moja kisha anakabidhi halmashauri ya Manispaa ya Songea.Hata hivyo wajumbe walihoji juu ya ujenzi huo na ukubwa wa eneo kulingana na ongezeko la watu, magari na huduma nyinginezo katika eneo hilo kuwa haliwezi kukidhi ongezeko hilo kutokana na eneo hilo kuonekana dogo.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiendelea kuhoji juu ya ujenzi wa kituo hicho kipya  cha Mabasi ambacho kimezua utata miongoni mwa wajumbe hao.
Toka kushoto ni katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamedi Maje akiwa na mjumbe kutoka wilayani Tunduru wakiwa wameshikwa na butwaa baada ya taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa kituo hicho cha Mabasi
Kaimu Mhandisi wa Manispaa ya Songea Davis Mbawala  akijibu maswali ya wajumbe juu ya ujenzi wa kituo kipya cha mabasi kinachojengwa kwa mfumo wa JENGA,ENDESHA,KABIDHI,
Toka kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga, Mwandishi wa habari wa ALAT mkoa wa Ruvuma Nathan Mtega na mkurugenzi wa Halmashauri ya Namtumbo ambaye pia ni Katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamed Maje wakiwa katika picha ya pamoja
Katibu wa ALAT mkoa wa Ruvuma Mohamed Maje akiteta jambo na Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga wakati wa majumuisho ya ziara ya wajumbe wa ALAT baada ya ukaguzi wa miradi
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania(ALAT) Mkoa wa Ruvuma wakiwa ndani ya ukumbi wa mkutano
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru akitoa hoja katika kikao cha majumuisho baada ya ziara ya kukagua miradi
Mwandishi wa habari Cresencia Kapinga akitoa mapendekezo katika kikao cha majumuisho.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Tunduru Robert Nehata akiuliza swali
katibu ALAT Mohamed Maje akizungumza kabla ya kumkaribisha mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho