Sunday, April 7, 2013

JESHI LA POLISI SONGEA LAWASAMBALATISHA MADEREVA PIKIPIKI KWA MABOMU

   Picha siyo ya tukio

Na Amon Mtega,
      Songea.

  JESHI la polisi mkoani Ruvuma  juzi limelazimika kuwatawanya kwa mabomu  madereva pikipiki maarufu kwa jina la yeboyebo wa manispaa ya Songea mkoani humo baada ya madereva hao kuandamana kuleekea kituo cha polisi cha mjini hapo kwa lengo la kushinikiza jeshi hilo liwaachie madereva wenzao wawili walioshikwa na pikipiki zao kufuatia makosa waliokutwa nayo.



 Akiongea na kwa njia ya simu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimek alisema kuwa mabomu hayo ya kuwatawanya yalitumika kufuatia vitendo vya madereva kutaka kuzuia kazi ya polisi katika utendaji wake usifanikiwe.



 Tukio hilo lilitokea April 5 mwaka huu  majira ya saa 11.30jioni katika kituo kikuu cha polisi kilichopo mjini hapo baada ya madereva hao kuandamana na mapikipiki yao kwa lengo la kushinikiza wenzao wawili  walioshikwa  na pikipiki zao kufuatia makosa waliokutwanayo kwenye pikipiki hizo kinyume na sheria za barabarani na kulitaka jeshi hilo liwaachie.



 Nsimek alisema kuwa kinachofanywa na madereva pikipiki hao hakiwezi kukubalika kwa kuwa ni kinyume cha sheria cha kulizuia jeshi la polisi linapofanya kazi yake na kuwafanya wananchi washindwe kupata huduma ya usalama na mali zao kikamilifu.



  “Mimi kama kamanda siwezi kukubaliana na baadhi ya vitendo vinavyofanywa na madereva pikipiki hao kwa kutaka wao waonekane wapo juu ya sheria jambo ambalo haliwezekani kabisa ni lazima kila mmoja atii sheria bila suluti”alisema kamanda huyo.



  “Naomba madereva pikipiki wanielewe kwamba ni lazima sheria zifuatwe na siyo mambo wanayoyataka ya kushindana na jeshi la polisi bila sababu za msingi na kuwafanya wananchi waishi katika hali ya hofu”alisema Kamanda Nsimeki.



   Aidha kamanda huyo hakuweza kuwataja majina ya madereva pikipiki waliokamatwa kwa makosa yaliyodaiwa kuwa ni uzembe barabarani kwa kuwa jeshi hilo linaendelea kulifanyia kazi.  



Kwa upande wao wananchi waliokuwa wakitimua mbio kufuaatia mabomu hayo ambao majina yao hayakutambulika walisikika wakisema kuwa  sasa serikali inatakiwa iangalie upya namna ya utoaji elimu kwa madereva pikipiki hao pamoja na kuzitambua sheria ili kuepusha malumbano ambayo yameshaanza kuota sugu.