Wednesday, April 3, 2013

TAASISI YA BENJAMINI WILLIAM MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION YAENDELEA NA UHAMAMISISHAJI WA AJIRA KATIKA SEKTA YA AFYA NCHINI KWA WANAFUNZI WA VYUO VYA AFYA VILIVYOPO KATKA MANISPAA YA SONGEA MOANI RUVUMA.


Kaimu katibu tawala mkoa wa Ruvuma ndugu Severine Tossi kushoto akiwa na Mratibu wa kanda nyanda za juu kusini Bi Atuganile Jonas   katika unguzi wa uhamasishaji wa ajira katika sekta ya afya nchini kwa wanafunzi wa vyuo vya afya mkoani Ruvuma.

Katibu wa Afya manispaa ya Songea mjini Bw. George Mhina akifatilia kwa makini washa ya uhamasishaji wa ajira katika sekta ya afya nchini kwa wanafunzi wa vyuo vya afya mkoani Ruvuma
.................................................

Taasisi hii ya Benjamini William mkapa HIV/AIDS  imeendela kwa kuandaa maonyesho  ya uhamasishaji wa  ajira katika sekta ya afya nchini kwa wanafunzi na wahitimu wa vyuo vya afya katika manispaa ya songea.

Kwa hivi sasa sekta ya afya inakabiliwa na upungufu wa wataalam wa afya sehemu zote nchini lakini hali hii imeathiri zaidi sehemu za vijijini ambako ndiko waliko watanzania wengi.Kutokana na hali hiyo serikali nayo imeweza kujipanga ikishirikiana na wadau  mbalimbali ili kuweza kuinusuru hali ngumu ya kutokuwa na wataalamu wa kutosha.

Mikakati na miongozo mbalimbali inatekelezwa ikiwemo mpango Mkakati wa tatu wa Sekta ya Afya(Health Sector Sector Strategic Plan).Mipango iliyoainishwa  kwenye mikakati hii ni pamoja na kuweza kuhakikisha  kuwa wanapatikana wataalamu wa kutosha  ili waweze kuajiriwa na kutoa huduma zenye ubora kwa wananchi walio wengi. Hii ni pamoja na kuahamasisha wataalam wanaohitimu katika vyuo vya mafunzo waweze kuajiriwa katika sekta ya afya ili kuweza kuongeza idadi ya wataalamu wanaotoa huduma.

 Katika  hutuba iliyotolewa na Kaimu katibu tawala mkoa wa Ruvuma ndugu Severine Tossi katika chuo cha maafisa tabibu songea amesema malengo ya uhamasishaji huu ni kuelimisha juu ya nafasi za ajira katika  halmashauri za wilaya katika mkoa wa Ruvuma , Maboresho yaliyofanyika katika sekta ya afya na maslahi ya mfumo wa utunzaji, upatikanaji na ubadilishaji wa taarifa za wahitimu kati ya vyuo na waajiri (wizara husika na Halmashauri).

“ Ninaomba niwaase wanavyuo kuwa serikali inajitahidi kuboresha maslahi ya watumishi wake wote pamoja na wa sekta ya afya, Sisi ni mashuhuda  na tumeona  ni jinsi gani basi ajira katika sekta ya afya imeongezeka  mwaka hadi mwaka, pia imeendelea kutambua kada ambazo hapo awali hazikuwepo . Hii ni ishara kuwa serikali inajali na hivyo mna kila sababu za kukata shauri la kujiunga na sekta ya  afya”

Nae Atuganile Jonas ambaye ni Mratibu wa kanda nyanda za juu kusini amesema mbali na zoezi la uhamasishaji wa ajira katika halmashauri za mikoa mbalimbali hapa nchini Tanzania pia wameajili wa tumishi wa afya amabo wamepelekwa kwenye halmashauri mbalimabali “watumishi hao wapo chini ya taasisi kwa mkataba maalumu baada ya hapo halmashauri husika uwauwisha katika ajira ya serikali na kuwa watumishi wa umma”

Atuganile ameongezea kwa kusema taasisi hii ya Benjamini William mkapa HIV/AIDS Foundation inamradi wa ujenzi wa nyumba katika halmashauri sabani  katika mradi huo halimashauri moja hujengewa nyumba kumi mpaka sasa mkoani mtwara na lindi tayali wameshakamilisha na kukabidhi  nyumba hizo.

Na kwa mkoa wa  Rukwa na Katavi nyumba zimeshakamlika bado makabidhiano na kwa upandea wa mkoa wa Ruvuma halmashsuri nne zitajengewa nyumba kumi kwa kila halmashaur moja ,nakati ya halmashauri hizo ni mbinga , namtumbo. Tunduru,songea vijijin,

Vilevile taasisi ya Benjamini William mkapa HIV/AIDS  Wanaufadhiri wa wanafunzi ambao wanaoenda kusoma katika vyuo vya afya kwa wale ambao wamefauru kwa kiwango lakini hawana uwezo kutokana na hali zao za kimaisha , Hadi sasa wanafunzi 150 wapo vyuooni kutokana na taasisi hii imeingia mkataba na halmasharu pamoja na wanafunzi kwa kuwapa msaada wa kuwaghalamikia masomo na baada ya kumaliza masomo yao watarudi katika halmashauri zao na kufanya kazi .