Friday, April 19, 2013

Watoto 250 wanaoishi katika mazingira hatarishi Songea wasaidiwa bima ya afya

Na Nathan Mtega,Songea.
JUMLA ya watoto 250 wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wanaoishi katika mazingira hatarishi jana wamepata kadi za mfuko wa afya kwa jamii [CHF]zitakazofanya watibiwe bure kwa muda wa mwaka mmoja .
 
 Watoto hao wamekabidhiwa kadi hizo kupitia shirika lisilo la kiserikali la ROA linalo fanyakazi ya kuwahudumia watu waishio katika mazingira hatarishi ikiwemo na wagonjwa waliopo majumbani mkoani hapo.
 
 Awali Mwenyekiti wa shirika hilo Mathew Ngalimanayo akitoa taarifa mbele ya mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti ambaye alikuwa mgeni rasmi ka zoezi hilo la ugawaji wa kadi hizo kwa watoto hao alisema kuwa shirika hilo linafanya kazi ya kuwahudumia watu waishio katika mazingira hatarishi na wagonjwa majumbani.
  Ngalimanayo alisema kuwa shirika hilo mpaka sasa limeweza kusaidia watoto 613 waishio katika mazingira hatarishi na kuwa pia wanafanya kazi ya kuwapima afya kwa baadhi ya watu wanaohitaji kujua mwenendo wa afya zao hasa katika ugonjwa  hatari ya ukimwi.
 
   Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti akipokea taarifa hiyo alisema kuwa shirika hilo limeonyesha njia namna ya uhudumiaji wananchi waishio katika mazingira hatarishi tofauti na baadhi ya taasisi ambazo kazi yake zikipata fedha kwa wafadhili ni kula.
 
  Mkirikiti alisema kuwa taasisi za mtindo huo ni lazima azifute kwenye wilaya yake kwa kuwa hazifanyi kazi ambayo ilitarajiwa na wafadhili wanaowapatia misaada mbalimbali ikiwemo ya fedha.
 
  Alisema kuwa hatanii atazifungia hizo taasisi kwa kuwa zinajinufaisha kupitia migongoni mwa watu waishio katika mazingira hatarishi kwa kutowasaidia kama maeelekezo ya maombi yao kwa wafadhili waliowapatia misaada.
 
Alisema kuwa hajapata kuona taasisi inayohudumia na kufuata taratibu zilizowekwa na wafadhili kama shirika hilo la ROA na kutaka asasi nyingine zisizo za kiserikali  kuiga mfano wa shirika hilo.alima mkuu huyo wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti.
 
Mwisho.