Thursday, April 4, 2013

UCHU WA MADARAKA WAWAKUMBA VIONGOZI WA CCM - TUNDURU

Na Steven  Augustino, Tunduru

WAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM) kikidai kujipanga kuunganisha na kuimarisha nguvu kwa viongozi wake nchini Wilayani Tunduru Mkoni Ruvuma hali imekuwa ni tofauti baada ya viongozi wa chama hicho kuanzisha mgogoro wa kugombania kubadilishana cheo.
Hayo yamebainika kufuatia kuwepo kwa mvutano huo wa chini kwa chini kushindwa kupatiwa dawa na uongozi wa CCM Mkoa na Wilaya juu ya madai ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (Mneki) Alhaji Ajili kalolo kutaka kubadilishana Cheo chake hicho na Mweyenkiti wa Ccm Wilaya ya Tunduru Bw.Hamisi Kaesa. 

Kufuatia hali hiyo hivi sasa Mwenyekiti wa CCM Wilaya amedaiwa kuwa amekuwa akilazimika kuvunja itifaki hiyo na maelekezo ya Chama na kumpisha mneki huyo akae kiti cha mbele ili aweze kujiridhi katika roho yake.


Taarifa za malumbano hayo yaliyosababisha kuzuka kwa mgogoro huo pamoja na matukio ya vitisho vya maneno makali na vijembe miongoni mwa viongozi hao yanadaiwa kuanzisha na Alhaji kalolo ambaye inadaiwa kuwa anahitaji kutukuzwa na kupishwa akae mbele kwa lengo la heshima ya kuonekana kuwa yeye ndiye anayepeperusha Bendera ya Chama hicho kaatika misafara yote.  

Suala hilo ambalo limezua utata na kusababisha mtafaluku mkubwa kati ya viongozi hao linadaiwa kuwa chanzo chake ni Mneki huyo kutoridhishwa na kukubaliana na maelekezo ya itifaki za chama chake zinazoelekeza kuwa Viongozi wote wenye nafasi na cheo kama chake inawataka kukaa kiti cha nyuma cha gari inapotokea yeye na mwenyekiti huyo wanasafiri kwa pamoja.

Aidha taarifa hizo zilizo dhibitishwa na viongozi wa CCM Wilaya ya Tunduru na Mkoa wa Ruvuma ambao waliomba wasitajwe majina yao gazetini zinaeleza kuwa Bw. Kalolo ambaye mahitaji yake wakati wa kuingia katika mchakato huo  yalikuwa ni kutafuta heshima na kutukuzwa hivi sasa anajutia na kuulaumu uongozi uliopita katika chama hicho kuwa walimuuza kutokana na kumshawishi agombee nafasi hiyo ambayo inaonesha kutokidhi haja za malengo yake.

Alipotakiwa kuzungumazia mgogoro huo Mweenyekiti wa CCM Wialaya ya Tunduru Bw. Hamisi Kaesa alisema kuwa tatizo hilo kwa sasa ni kubwa na haelewi jinsi ya kuliepuka kutokana nay eye kutokuwa na mamlaka ya kubadilishana nafasi hizo zaidi ya maamuzi ya kura zilizopigwa na wajumbe wa mkutano mkuu ulio wachagua.
  “tatizo hili ni kubwa na hivi sasa kuna mgogoro mkubwa kati yangu na Mneki, lakini hivi sasa mimi nimekuwa nikijishuhsha na kumpisha yeye akae kiti cha mnbele ili aweze kujiidhisha nafsi yake ingawaje mimi na viongopzi wa chama Wilayani tumekuwa tuki kiuka miongozo na itifaki ya Chama” alisema Kaesa.

Juhudi za kumtafuta Mjumbe huyo wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (Neki) alihaji Ajili Kalolo ili aweze kujibu tuhuma hizo hazikuzaa matunda kutokana na kutopatikana katika simu yake
 Mwisho