Saturday, April 6, 2013

KAIMU MKUU WA MKOA WA RUVUMA JOSEPH JESEPH MKIRIKITI AWATAKA WAKULIMA KUFATA KILIMO CHA KISASA


Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa wilaya Mh.Joseph Joseph Mkirikiti akisisitiza jamba kwa wanakijiji wa Palangu alipo tembele shamba la mkulima Bw. Isaya Mwilamba
Mmilikiwa Shamba Bw. Isaya Mwilamba akimwelekeza siri ya mafanikio yake ya kujiwekeza katika kilimo chake kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh.Joseph Joseph Mkirikiti

Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh. Joseph Joseph Mkirikiti akionyeshwa jinsi mhindi beba punje za mahindi vizuri katika shamba la muwekezaji


Shamba la muwekezaji lenye ukubwa hekali 250
 Mmiliki wa Blog ya demashonews toka kulia akiwa na mwandishi wa habari wa Star TV Adamu Nindi nao walikuwepo katika kuchukua habari
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Ruvuma akiwa ameongozana na wadau mbalimbali pamoja na mmiliki wa Shamba akikagua shamba 
Hii ndio Hotel anayo miliki kutokana na uwekezaji wa kilimo
 
..............................................................................

Kaimu mkuu wa mkoa wa ruvuma ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya songea Joseph Joseph  Mkirikiti amefurahishwa na mkulima wa mjini   humo  Bw . Isaya Mwilamba  ambaye amepata mafanikio makubwa kupitia kilimo cha kisasa na kuwataka wakulima wengine kumuiga mkulima huyo.

Alionyesha kufurahishwa na mkulima huyo baada ya kutembea shamba la mkulima huyo lenya ukumbwa zaidi ya hekali 250 ambalo limestawi vizuri kutokana na kulima kwa kufuata kanununi bora za kilimo na kuzingatia matumizi ya mbegu bora.

Kaimu Mkuu wa mkoa huyo akizungumza katika kijiji cha palangu songea vijijini ambako mkulima huyo amelimia shamba hilo alisema mambo mazuri haya fanywi na wazungu pekee kwani mkulima huyo  ameonyesha wa tanzania wanaweza kufanya mambo makubwa
  “ Jamani wenyewe simumeona hili shamba limelimwa na wazungu?  Ni kweli wakulima wengine mnapaswa kumuiga Mwilamba ambaye amepata  mafanikio makubwa kupitia kilimo na kujenga hotel ya kisasa yenye thamani ya kuzidi  bilioni moja “

Kwa upande wake mmoja wa wakulima wakubwa wa mkoa wa ruvuma Bw. Isaya Mwilamba ameiomba serikali kuanzisha Bank ya wakulima na kubainisha kwamba  bank hiyo itakuwa ni mkombozi kwa wakulima kwa kuwa itakuwa ikitoa mkopo kwa mashariti nafuu kuliko bank zilizopo sasa  ambazo zinamuona mkulima ni mtu asiekopeshaka .

Mkulima huyo amefafanua kuwa bank zilizopo sasa zimekuwa zikimtaka mkulima aonyeshe hati ya nyumba  pindi anapotaka kukopa kwenye bank hizo wakati wakulima waliowengi hawana hati za nyumba  na pia hawana nyumba bora ambazo zinaweza kuwa dhamana ya mkopo.