Saturday, April 6, 2013

PAMBANO LA NGUMI KUFANYIKA AGOSTI 8 MWAKA HUU - SONGEA MKOANI RUVUMA


Na Fulmence Mbunda,Songea

MABONDIA wa ngumu wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wameanda pambano la ngumi agosti 8 mwaka huu ilikuwata wapenzi na wadau wa mchezo huo wawaeze kutoa hudhamini wa michezo hiyo,ambao utafanyika kwenye uwanja wa maji maji songea mjini.


     Mmoja wa washiriki mkuu wa mchezo huo Mussa Omary alisema kuwa pambano hilo wameanda wakiwa na lengo kubwa la kutafuta hudhamini katika michezo ya ngumi kwa kuwa wadau wengi wameusau mchezo huo jambo ambalo wanashindwa hata kwenda kushiriki mashindano mbalimbili ya mchezo huo.


    Alisema kuwa pambano hilo litakuwa ni moja ya kuwapatanisha baadhi ya wanamichezo wa ngumi na kuwataka kuwa wabunifu wa kuweza kujishirikisha na mambo mbalimbali ikiwa ni moja ya kuendeleza ngumi katika mkoani humo na kwa kuwa maporomota wengi kuwa feki ambapo jambo lingine linalo wachangia kukosa kwa wadhamini.


    “tumeanda pambano sisi wenyewe ambalo litakuwa nzuri na lengo kubwa la kuandaa pambano hilo kwanza kuwataka wanadau na wapenzi wa ngumi waweze kutuchangia ,pili ikiwa ni moja ya kuwakutanisha mabondia wa ngumi hasa mkoani hapa kwa kuwa mabondia wamekuwa maporomota feki wanaweza kuandaa pambano lakini wanashindwa kufuata utaratibu hivyo pambano hilo litakuwa la kuwalekebisha baadhi ya mabondia.”alisema Omary

    

    Hata hivyo Omary alimtaja bigwa ambaye atapigana naye siku ya pambano hilo kuwa ni Oborti Ameme wa kutoka Mbeya ambapo alisema kuwa yeye anashikiria mkanda wa Taifa kwa kuwa na kilo 59 na huyo bondia toka Mbeya hanarekodi yeyote na Saimoni Mwakwenda  atapigana na Maisha Samsoni wa kutoka Mbeya.


     Omary aliwataja mabondia wengine ambao watashiriki mchezo huo kuwa ni Alibabu wa songea na Kenedi Kitenge wa  kutoka Iringa,Sunusa Bakari wa songea na Taisoni wa kutoka Mbinga na Jemusi Mtanga wa Songea na Furaha Tengeni wa kutoka wilaya ya kyera.


    Hata hivyo omary aliwataka wadau na wapenzi hasa wakiwemo viongozi wa mkoani hapa  kutoa hudhami wa michango mbalimbali ili kuweza kukuza  na kuendeleza mchezo wa ngumi ikiwa mchezo huo ni mchezo hunao pendwa na watu wengi katika sehemu mbalimbali.