Monday, April 22, 2013

Wawili wafariki dunia katika ajali ya gari

Na Nathan Mtega,Songea
 WATU wawili wamefariki dunia na mmoja akijeruhiwa  katika ajali ya gari iliyotokea Aprili 21 mwaka huu majira ya saa 11 jioni katika eneo la Wino wilayani Songea mkoani Ruvuma katika bara bara ya Songea-Njombe.
 Ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Scania yenye namba za usajili T 974 ANN iliyokuwa ikiendeshwa na dereva Festo Elia  Kimata(29) ilipata ajali hiyo katika eneo la Wino mtelemkoni kwa kile kilichoelezwa kuwa dereva wa gari hilo alishindwa kuimudu kona hiyo hali iliyosababisha gari kupinduka na yeye  kufariki dunia papo hapo.
 Mtu mwingine aliyefariki dunia katika ajali hiyo ni Fausta Mlelwa(35) mkazi wa kijiji cha Kifagulo kilichopo katika eneo la Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma huku utingo wa gari hilo Lufinus Mayemba(32) akijeruhiwa vibaya na kulazimika kukimbizwa katika hospitali ya Misheni ya Peramiho kwa ajili ya matibabu.
 Ajali hiyo imetokea saa chache baada ya ajali nyingine iliyotokea katika eneo hilo iliyohusisha gari aina ya NOAH iliyokuwa ikitokea mjini Songea kuelekea jijini Mbeya ambayo ilisababisha watu kunusurika kifo kwa kujeruhiwa nba kulazwa katika hospitasli ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kwa matibabu.
 Kufuatia kuwepo kwa ajali za mara kwa mara katika eneo hilo baadhi ya wananchi wameiomba  wakala wa bara bara(TANROAD) mkoa wa Ruvuma kuboresha alama za bara barani katika eneoi hilo na pia serikali kuona uwezekano wa kukiboresha zaidi kituo cha afya cha afya cha Madaba eneo ambalo limekuwa na ajali nyingi.
 Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki akitihibitisha kutokea  kwa ajali hiyo kwa njia ya simu alisema anawasiliana na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ili kuona uwezekano wa kufanyia lazi maombi ya wananchi hao.
Mwisho.