Monday, April 8, 2013

TEMBO WAENDELEA KUTEKETEZWA MKOANI RUVUMA

 

  Kamanda wa polisi Mkoani Ruvuma Deusdedit Nsimek akizishika nyara za serikali hizo ambazo zimekamatwa(mikia ya tembo)
..................................................................................................
JESHI la polisi mkoani Ruvuma  linamshikilia mtu mmoja  ajulikanae  kwa jina la Bakari Said [17]mkazi wa kijiji cha mbalakiwa kata ya Ligunga wilaya ya Tunduru mkoani humo kwa tuhuma ya kukutwa na mikia 10 ya Tembo  ambayo ni nyara za serikali  huku ikikadiliwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 247.
  Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimek amesema kuwa tukio hilo la kumkamata mtuhumiwa huyo lilifanyika April 5 mwaka huu majira ya saa 7.15 usiku kwenye Nyumba anayoishi mtuhumiwa huyo katika kijiji cha mbalakiwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema wa kijiji hicho.
   Kamanda amesema kuwa kumekuwepo kwa vitendo vya kijangili dhidi ya nyara za serikali kwa majangili hao kuuwa wanyama mbalimbali hasa Tembo na kuchukua pembe zao kwa malengo ya kwenda kufanya biashara kinyume na taratibu za kisheria .
     Amesema kuwa licha ya mtuhumiwa huyo kutambuliwa akiwa na umri wa miaka 17 lakini sheria itachukua mkondo wake ilikubaini na wengine wanaofanya vitendo hivyo .
      “Kwa hali hii niwazi kuwa Tembo 10 wamepotea kwa kuuwawa  pamoja pembe zake 20 jambo ambalo limeisababishia hasara serikali kiasi cha fedha kilicho kadiliwa kuwa ni shilingi milioni 247kwa fedha ya kitanzania’alisema Kamanda huyo.
          Aidha kamanda amesema kuwa mtuhumiwa tayari anatarajiwa kufikishwa mahakamani ili kujibu shistaka linalo mkabili na kuwa aliwaomba wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kuwafichua watu wanaofanya vitendo hivyo vya kulihujumu taifa.
                        MWISHO.