Tuesday, April 9, 2013

MADEREVA DALADALA WAGOMA SONGEA

Hapa ni stendi ya daladala ziendazo Luwiko, Namanditi na Lilambo gari likiwa tupu kufuatia mgomo wa madereva .

Na Amon Mtega, Songea.

MADEREVA wa gari za abiria maarufu kwa jina la daladala zinazofanya safari katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma LEO wamegoma kutoa huduma kwa muda zaidi ya masaa mtatu kufuatia  baadhi ya madereva kunyang’anywa leseni ,kutolewa  namba za magari hayo pamoja kubadilishwa kwa vituo vya kupakia na kushusha abiria.

 Tukio hilo limetokea jana katika kituo cha daladala kilichopo maeneo ya Ikweta katika manispaa hiyo na kusababisha usumbufu kwa abiria ambao walikuwa ndani ya daladala hizo kushindwa kusafiri kwa kulazimishwa kushuka kabla ya safari zao na kumfanya mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti  pamoja na timu yake  kuingilia kati kumaliza mgogoro huo.

  Madereva hao wakimueleza mkuu wa wilaya kufuatia mgomo huo  walisema kuwa waliamua kugoma kufuatia baadhi ya madereva wenzao kunga’anywa leseni ,kutolewa  namba ya gari,kunyanyashwa na baadhi ya askari polisi wa usalama barabarani kwa kuzabwa vibao pamoja kubadilisha baadhi ya vituo vya daladala hizo.

  Kwa upande wake kaimu  mkuu wa mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti akitatua mgomo huo aliwataka   madereva hao waendelee na kazi ya utoaji wa huduma ya usafirishaji abiria kwa kufuata sheria zinazo takiwa huku aliondoka na viongozi wa madereva hao kwenda kujadili suala hilo kwa pamoja.

  Akiongea na viongozi wao katika ukumbi wa ofisi yake kaimu  mkuu wa mkoa huo alisema kuwa hakuna sababu za kufanya mgomo kwa kuwa sheria za usalama barabarani zipo na zinatakiwa zifuatwe bila shuluti na kuangalia vituo vilivyo kataliwa askari wa usalama maana vituo hivyo havipo maeneno salama.

    “Kitendo mnacho dai kuwa mnanyanyaswa kwa kupigwa na kunyang’anywa leseni litaangaliwa kwa kulifanyia kazi lakini kilichopo ni kuhakikisha leseni zenu ziwe zenye sifa ya kubeba abiria “alisema mkuu huyo.

      Naye kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki alisema kuwa yeye anafuata sheria ni lazima sheria za usalama  barabarani zifuatwe na kuwa kama kuna askari usalama barabarani anapokea rushwa kutoka kwa madereva hao basi sheria ichukue mkondo wake .
                  MWISHO.